Thursday, July 26, 2012

Azania Bank gives 65m/- to supports slam upgrading project

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI MHE. DKT. CHARLES TIZEBA (MB) AFANYA ZIARA KATIKA BANDARI YA DAR ES SALAAM JANA


Meneja Msaidizi wa Bandari ya Dar es Salaam, Bi. Winnie Mulindwa, akitoa taarifa ya namna Bandari ya Dar es Salaam inavyofanya kazi kwa Naibu Waziri wa Uchukuzi, Dkt. Charles Tizeba (aliyeshika kichwa), ambaye amefanya ziara ya siku moja katika Bandari ya Dar es salaam. Kushoto kwa Naibu Waziri ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Mhandisi Omar Chambo, Kulia kwa Katibu Mkuu ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo,Bw. John Mngodo, Kushoto kwa Meneja Bandari Msaidizi ni Mkurugenzi wa Idara ya Usalama na Mazingira kutoka Wizara ya Uchukuzi,Bi. Tumpe Mwaijande.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya kupakua na kupakia makontena Bandarini (TICTS), Bw. Neville Bisett akifafanua jambo kwa Naibu Waziri wa Uchukuzi, Dkt. Charles Tizeba (Mwenye Suti ya Mikono Mifupi),wakati alipofanya ziara ya siku moja kuangalia ufanisi wa Kampuni hiyo katika Bandari ya Dar es Salaam leo.Kulia kwa Naibu Waziri ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi,Bw. John Mngodo.

Naibu Waziri wa Wizara ya Uchukuzi, Dkt. Charles Tizeba akifafanua jambo kwa uongozi wa Wizara, Bandari na Mkurugenzi Mtendaji wa Kitengo cha Kupakia na kupakua makontena TICTS, kulia kwa Naibu Waziri ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Bw. John Mngodo, Kushoto kwa Naibu Waziri ni Meneja Msaidizi wa Bandari ya Dar es Salaam, Bi Winnie Mulindwa, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo(aliyevaa tai ya blue), Mhandisi Omar Chambo, na Kulia kwa Katibu Mkuu ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Kupakua na Kupakia Makontena (TICTS), Bw. Neville Bisett.


Naibu Waziri wa Uchukuzi,Dkt. Charles Tizeba (Mb),akiongea na baadhi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania(hawapo pichani),wakati alipotembelea Taasisi hiyo leo jijini Dar es Salaam,Kushoto kwa Naibu Waziri ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Mhandisi Omar Chambo, Naibu katibu Mkuu wa Wizara hiyo (wa pili kushoto),Bw. John Mngodo. Na aliyevaa Kizibao ni Meneja Msaidizi wa Bandari ya Dar es Salaam,Bi. Winnie Mulindwa.(Picha Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-Uchukuzi)



Bajeti ya Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia yapitishwa kwa mwaka 2012/13

Watu wazidi kujinyakulia zawadi za promosheni ya VUMBUA HAZINA CHINI YA KIZIBO ya SBL


SERIKALI IMESEMA HAIJADHULUMU MALIPO YA WAHANGA


ZITTO KABWE:NISIHUSISHWE NA MATAMSHI NA MAKANUSHO WA WABUNGE WALIOKUWA KIGOMA


Mafunzo 1st EAC-GIZ Masterclass Photography yaendelea Arusha


MAADHIMISHO YA SIKU YA KUMBUKUMBU YA MASHUJAA VIWANJA VYA MNAZI MMOJA JIJINI DAR ES SALAAM LEO


RAIS WA ZANZIBAR DKT SHEIN AMUAPISHA WAZIRI WAZIRI MPYA WA MIUNDOMBINU BAADA YA WA AWALI KUTANGAZA KUJIUZULU JUZI




Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein, akimuapisha Rashid Seif Suleiman, kuwa Waziri wa Miundombinu na Mawasiliano, wakati wa  hafla fupi iliyofanyika Ikulu Mjini Zanzibar jana

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein, akimuapisha Sheikh Daudi Khamis Salim,  kuwa Kadhi wa Rufaa Pemba, wakati wa hafla iliyofanyika Ikulu Mjini Zanzibar jana.
Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi, akisalimiana na Viongozi waliohudhuria katika hafla ya kiapo cha Waziri Mpya wa Miundombinu,Rashid Seif Suleiman, katika Ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar Jana.Picha na Ramadhan Otrhman,Ikulu

No comments:

Post a Comment