
Mwanamuziki muimbaji Rehema
Chalamila maarufu kama RayC amekumbwa na tatizo kubwa la kuathirika na
madawa ya kulevya. Kwa sasa yumo katika hatua za matibabu ya kujaribu
kuondokana na tatizo hilo.
Kwa kadri ya maelezo ya mama yake
dawa ambazo anahitaji kuzitumia ili kuponi ni gharama na pia kama wote
tunavyofahamu pia mgonjwa yoyote anatakiwa kula vizuri, mzigo huu ni
mkubwa kwa huyu mama, kwa hiyo kunahitajika msaada wa kubeba mzigo huo.
Wapenzi wa muziki wa binti huyu na
watu wenye mapenzi mema tunaweza kumsaidia mama huyu kwa kumtumia kiasi
chochote cha fedha kwa kutumia huduma ya tigo pesa kupitia namba
0655999700
Natanguliza shukrani kwa wote watakao weza kutoa msaada wowote kwa ajili ya matibabu ya mwenzetu
Habari hii kwa hisani ya Mzee Kitime-Mwanamuziki Mkongwe hapa nchini.
RAIS KIKWETE AMPA POLE KATIBU WA MUFTI WA ZANZIBAR ALIYEMWAGIWA TINDIKALI


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimjulia hali na kumpa pole Katibu wa
Mufti wa Zanzibar Sheikh Fadhili Soraga ambaye amelazwa katika chumba
cha dharura katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kufuatia majeraha ya
usoni na kifuani yaliyotokana na kurushiwa Tindikali na watu
wasiojulikana wakati akifanya mazoezi katika Kiwanja cha Mwanakwerekwe
mjini Unguja juzi. Rais ambaye amerejea leo Jumanne Novemba 6, 2012
akitokea katika ziara ya kikazi ya takriban juma moja katika mikoa ya
Kilimanjaro, Arusha, Manyara na Singida, amemtakia Sheikh Soraga nafuu
ya haraka.PICHA NA IKULU
KUTOKA VIWANJA VYA BUNGENI MJINI DODOMA JANA
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Mbunge wa Kibakwe na Naibu Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene, Bungeni Mjini Dodoma Oktoba 6, 2012. |
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiteta na Mbunge wa Maswa Magharibi, John Shibuda Magalle kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma, Oktoba 6,2012. |
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiongea na Mbunge wa Mpedae, Salim Hassan Abdullah Turky kwenye viwanja vya Bunge Mjini Dodoma,Oktoba 6, 2012.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) |
MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AFUNGUA MKUTANO WA 8 WA KIMATAIFA WA BIMA JIJINI DAR JANA

Makamu
wa
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
akihutubia wakati akifungua mkutano wa 8 wa Kimataifa wa Bima, ulioanza
leo katika ukumbi wa Blue Peal, jijini Dar es Salaam. Mkutano huo
unatarajia kumalizika Novemba 8 mwaka huu.
Baadhi
ya washiriki wa Mkutano huo wa Kimataiafa wa Bima, kutoka mataifa mbalimbali
wakimsikiliza Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed
Gharib Bilal, wakati akihutubia, katika ukumbi wa Blue Peal, leo.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
akifurahia ngoma ya asili wakati akiwasili kwenye Ukumbi wa Blue Peal, jijini
Dar es Salaam, leo kwa ajili ya kufungua mkutano wa 8 wa Kimataifa wa Bima,
ulioanza leo Novemba 6, 2012 ukitarajia kumalizika Novemba 8, mwaka huu.
BODABODA JIJINI MBEYA WAVAMIA KITUOCHA KUUZIA MAFUTA KWAAJILI YA KUHAKIKISHIWA KWELI HAKUNA MAFUTA AU YANAFICHWA

VIJANA WA BODA BODA WAKIWA WAMEVAMIA KITUO CHA ORXY KUTAKA KUJUA KAMA KWELI KUNA MAFUTA AMA LAH.
HAPA KILA MTU ANATAKA KUSHUHUDIA KAMA MAFUTA YAPO AMA LAH
MENEJA
WA KITUO HICHO ALIYE VAA SHATI JEUPE AKIJARIBU KUWATULIZA WATEJA AMBAO
WANA JAZBA KUBWA YA KUTAKA KUJUA KAMA KUNA MAFUTA AU LAH , NA KUWAMBIA
KUWA WANGOJE KWANZA ACHUKUE VIFAA ILI AWAONESHE KUWE KWELI HAKUNA
MAFUTA.
MKUU
WA POLISI WILAYA YA MBEYA NAE ALIKUWEPO ENEO LA TUKIO,KUWATULIZA VIJANA
HAO NA KUWAHAKIKISHIA KUWA WATAONESHWA KUWA KWELI HAKUNA MAFUTA KATIKA
ENEO HILO.
HAPA KATI KATI WANAPO TAZAMA NDIPO KWENYE TANK LA MAFUTA , VIJANA WANANGOJA KUSHUHUDIA.
Chama Cha Mapinduzi (CCM)Zanzibar:Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ifute Mara Moja Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu Zanzibar (JUMIKI)

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mkoa wa Mjini Magharibi, Borafya Silima.
---
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar
kimeitaka serikali ya Mapinduzi kuifuta mara moja Jumuiya ya Uamsho na
Mihadhara ya Kiislamu Zanzibar (JUMIKI) kwa kuwa inafanya kazi kinyume
na malengo yake usajili.
Kauli hiyo imetolewa jana katika mkutano
wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Mabata huko Magomeni Mjini
Unguja na kuhudhuriwa na wanachama wa CCM na wafuasi wa CUF ambapo mgeni
rasmi wa mkutano huo alikuwa ni Mwenyekiti wa Mkoa wa Mjini Magharibi
Borafya Silima.
Akizungumza katika mkutano huo Katibu wa
Vijana wa Mkoa wa Mjini Magharibi, Mohammed Ali Khalifa alisema chama
cha CCM kinamuomba msajili wa taasisi za kiraia achukue uamuzi wa
kuifuta jumuiya hiyo ya Uamsho ili isiwepo kabisa katika kumbukumbu za
asasi za kiraia hapa Zanzibar.
Alisema
taasisi hiyo haiendeshi shughuli zake za kidini licha ya kuwa
imesajiliwa kwa misingi ya kuendesha mambo ya dini lakini imepoteza
muelekeo na imekuwa ikifanya kazi za kisiasa jambo ambalo linakwenda
kinyume na malengo ya jumuiya hiyo.Aidha alisema Uamsho ina mkono wa watu
wakubwa ndani ya serikali na ndio muda wote imekuwa ukinyamaziwa na
hivyo kuitaka serikali kuwa macho na watendaji wake na kuwachukulia
hatua wale wote ambao wamehusika katika kuwaunga mkono na kuwakamta kwa
kuwafikisha katika vyombo vya sheria.
Kwa upande wake Mgeni rasmi wa mkutano
huo, Borafya Silima alisema jeshi la polisi limefanya kazi nzuri sana ya
kuhakikisha linawakamata wahalifu wote na kuwafikisha katika vyombo vya
sheria na kuwataka waendelee na kazi hiyo.
Borafya alisema haiwezekani viongozi wa
dini ambao hawana elimu kuachiwa kutamba na kuiharibu nchi kwa
kisingizio cha kutangaza dini wakati wanachokitangaza ni siasa huku
akikishutumu chama cha wananchi CUF kuwa kinahusika moja kwa moja na
vurugu zilizotokea kwa kuwabariki viongozi hao wa Uamsho.
“Mtu hana dini yenyewe haijui leo hii
tumwite sheikh kwani kuvaa kanzu ndio sheikh? Alihoji huku akishangiriwa
na wafuasi wa chama hicho.
Mwenyekiti huyo ambaye amechaguliwa hivi
karibuni amesema kwamba nafasi aliyopata ni muhimu katika siasa za
Zanzibar na kwamba ataitumia vizuri na kuwataka wapinzani wake wajipange
vizuri ili kukabiliana nao kwani wameingizwa madarakani kwa maridhiano.
Borafya alisema Maalim Seif amekuwa
amepewa wizara zisizo na uzito wowote serikali na hivyo amekuwa
akimuonea choyo makamo wa pili wa rais, Balozi Seif Ali Idd kwa kuwa
yeye ndio mshughulikiaji wa wizara zote za serikali.
Mazungumzaji katika mkutano huo ambao
kwa kiasi kikubwa wote waliohutubia walimlenga na kumshutumu moja kwa
moja Makamo wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad na
kumtaka aachie ngazi kwa kuwa ameshindwa kutekeleza yale ambao aliapa
kuyasimamia wakati akiingia madarakani.
Mbali na matusi ya nguoni na kumshutumu
kwamba anahusika na kundi la Uamsho walisema Maalim Seif hafai kuwa
kiongozi kutokana na kuwa mbinafsi kwa kuwa ameisema serikali yake mbele
ya viongozi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP) kwa
kuwaeleza kwamba jeshi la polisi na vikosi vya SMZ vinahitaji mafunzo ya
kukabiliana na vurugu ili waweze kupata mafunzo ya kukabiliana na
vurugu hizo bila ya kuvunja haki za binaadamu.
“Huyu Maalim Seif anawaambia UNDP kwamba
jeshi letu la polisi linahitaji mafunzo ya kuwakamata wahalifu sisi
tunamwambia polisi wetu na vikosi vyetu havihitaji mafunzo wewe ndio
unahitaji mafunzo kwa sababu kwani wewe unalindwa na nani? Si hawa hawa
polisi” alisema Khalifa.
Katika hatua nyengine viongozi hao wa
CCM walimtaka Maalim Seif kuachia ngazi kwa kwa kumsema rais wake Dk
Shein hadharani kitendo ambacho walisema ni kwenda kinyume na kiapo
chake cha kuheshimu, kulinda na kutotoa siri za serikali.
Hivi karibuni katika mkutano wake Maalim
Seif alimtaka Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohammed Shein kutekeleza ahadi
yake ya kuwalinda wananchi wote bila ya ubaguzi na kuhakikisha vyombo
vya ulinzi vinasitisha ukiukwaji wa haki za binaadamu kwa kuwa wananchi
wamechoshwa na ukandamizaji wanaofanyiwa katika nchi yao.
Katibu wa Mufti wa Zanzibar Sheikh Fadhil Soraga Amwagiwa Tindikali na Watu Wasiojulikana
Katibu wa Mufti wa Zanzibar Sheikh Fadhil Soraga akitolewa katika Chumba
cha Huduma ya Mwanzo katika Hospitali ya Mnazi Mmoja baada ya kurushiwa
Tindi kali na watu wasiojulikana wakati akifanya mazowezi huko katika
Kiwanja cha Mwanakwerekwe.
Katibu wa Mufti wa Zanzibar Sheikh Fadhil Soraga akipandishwa kwenye
Gari ya Wagonjwa kwa lengo la kuwahishwa katika Hospitali ya Muhimbili
Dare es Salaam baada ya kurushiwa Tindi kali na watu wasiojulikana
wakati akifanya mazowezi huko katika Kiwanja cha Mwanakwerekwe.
Wananchi mbalimbali wakishuhudia Katibu wa Mufti wa Zanzibar Sheikh
Fadhil Soraga akiwahishwa katika Hospitali ya Muhimbili Dare es Salaam
baada ya kurushiwa Tindi kali na watu wasiojulikana wakati akifanya
mazowezi huko katika Kiwanja cha Mwanakwerekwe.Picha na Yussuf Simai-Maelezo Zanzibar
No comments:
Post a Comment