Monday, January 14, 2013

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AENDESHA KIKAO CHA MUUNGANO MJINI ZANZIBAR LEO


 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiendesha Kikao cha Muungano, kilichofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Zanzibar Beach Resort, mjini Zanzibar leo, Januari 14, 2013. Wa pili (kushoto) ni Waziri Mkuu, Mizengo Pinda (wa pili (kulia) Ni Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Idd (kushoto) ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano), Samiah Suluhu na (kulia) ni Waziri wa nchi Ofsi ya Makamu wa pili wa Rais zanzibar, Mohamed Aboud. 
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiteta jambo na Makamu wa pili wa Rais, Zanzibar, Balozi Seif Ali Idd, wakati Makamu alipokuwa akiendesha Kikao cha Muungano kilichofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Zanzibar Beach Resort, mjini Zanzibar leo.
 Katibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Sazi Salula (kulia) Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Eng. Ngosi Mwihava (katikati) na Mkurugenzi wa Muungano, Rajab Baraka (kushoto) wakifuatilia vifungu katika machapisho ya kujadili masuala ya Muungano, wakati wa kikao cha Muungano, kilichoendeshwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal (hayupo pichani), kilichofanyika leo Januari 14, 2013, katika ukumbi wa Hoteli ya Zanzibar Beach Resort, mjini Zanzibar. 
 Baadhi ya Mawaziri wakiwa ukumbini humo wakati wakifuatilia kikao hicho cha Muumgano kilichoendeshwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, (hayupo pichani), leo katika Ukumbi wa Hoteli ya Zanzibar Beach Resort, mjini Zanzibar.
 Baadhi ya Mawaziri wakiwa ukumbini humo wakati wakifuatilia kikao hicho cha Muumgano kilichoendeshwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, (hayupo pichani), leo katika Ukumbi wa Hoteli ya Zanzibar Beach Resort, mjini Zanzibar.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Idd, na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Samiah Suluhu, mara baada ya kumalizika kwa kikao cha Muungano, kilichofanyika leo Januari 14, 2013 katika Ukumbi wa Hoteli ya Zanzibar Beach Resort, mjini Zanzibar.

WANAFUNZI IFM WAVAMIA WIZARA YA MAMBO YA NDANI NI BAADA YA KUKOSA ULINZI KWENYE HOSTELI, BAADA YA WENZAO WAKIUME WAWILI KUBAKWA NA MAJAMBAZI NA KULAZWA HOSPITALI. SAKATA LINAENDELEA KIGAMBONI MIDA HII CHINI YA USIMAMIZI WA KAMANDA KOVA


Wanafunzi wa Chuop Cha Uongozi wa Fedha cha jijini Dar es Salaam (IFM) wakiwa mbele ya geti la Wizara ya Mambo ya ndani walipovamia leo majira ya saa nne na nusu asubuhi wakiwa na madai ya kutopewa ulinzi na jeshi la polisi kwenye makazi yao ya Hosteli za Kigamboni kutokana na kuvamiwa na majambazi mara kwa mara. Wanafunzi hao walidai siku ya Ijumaa walifanya kikao na jeshi hilo ili wawape ulinzi lakini suala la ajabu siku waliyofanya kikao na Jeshi hilo ndio siku waliovamiwa wenzao wawili wakiume na kubakwa  hali iliyosababishwa wanafunzi hao kubakwa. Majambazi hao wamekua wakidai kupewa Laptop simu na fedha kama mwanafunzi akikataa humfanyia vitendo vya kulawiti.
Ulinzi uliimarishwa nje ya jengo la Wizara ya Mambo ya ndani kufuatia kadhia hiyo ya wanafunzi.
Kamanda wa Polisi wa Kanda maalum ya Kipolisi ya jiji la Dar es Salaam Suleiman Kova akimsikiliza Rais wa Serikali ya wanafunzi ya Chuo cha IFM mara baada ya kuwasili eneo la ofisi za Wizara ya Mambo ya ndani ambapo aliwaamuru wanafunzi hao wafuatane waende hadi Kigamboni kwenye Kituo walichoripoti taarifa zao pamoja na kwenda kwenye Hosteli zao. Kova aliahidi kushughulikia jambo hilo kwa haraka bila kusita.
"Wanafunzi wenzetu wa kiume wamelawitiwa nyinyi tumewapa taarifa siku ya ijumaa kuwa hatunaulinzi tunaibiwa hovyo vitu vyetu halafu siku hiyo hiyo unafanyika ubakaji huo"
Baadhi ya wanafunzi wakiwa kwenye mitaa ya Posta jijini humo wakielekea kwenye kivuko cha Kigamboni ili kwenda kumuonyesha Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Kipolisi ya jiji la Dar es Salaam Suleiman Kova.
Wakianza maandamano kuelekea Feli kwaajili ya kuvuka kwenda Kigamboni.
Kova akitoa maelezo kwa waandishi wa habari juu ya hatua zitakazochukuuliwa baada ya kupata taarifa hizo ambapo aliwaamuru wanafunzi hao wote kwapamoja kwenda Kigamboni kufuatilia tukio hilo kwa pamoja.
Mitaani Posta.
Hadi kieleweke!
Tunaimba! Tunavuka bure Tunavuka bure kwenye Pantoni.
Kova akishangiliwa wakati wa safari kuelekea Feli.
Kwenye Kona ya feli kuwania geti ili waingie bure!
Wakajazana kupita kiasdi Kova akazuia kivuko kisiondoke hadi wapungue!
Hapa wakigoma kupungua kazi iliyochukua zaidi ya Saa moja hadi kivuko kuendelea na kazi ya kuvusha abiria
Pamoja na kutakiwa kupungua hapa wengine walizidi kuendelea kuingia na kukijaza kivuko hicho. Picha zote na Raha za Pwani, hii ni sehemu ya kwanza tutawaletea sehemu ya pili ya tukio hili ambalo hadi hivi sasa filamu inaendelea hapa feli na ikielekea Kigamboni.Picha Kwa Hisani Ya Mtaa Kwa Mtaa Blog

mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya bia ya serengeti steve gannon atembelea mjengoni clouds media group.



Mkurugenzi Mtendaji wa Clouds Media Group,Joseph Kusaga 'Joe' pichani kushoto akichanganua jambo kwa Mkurungezi Mtendaji wa Kampuni ya bia ya Serengeti,Steve Gannon mara baada ya kutembezwa studio mpya na ya kisasa kabisa,iliyofungwa mjengoni humo,ambayo inatarajia kuanza kutumika hivi karibuni,Steve Gannon amefanya ziara fupi mwishoni mwa wiki na kutembelea vitengo vyote kampuni hiyo huku akijionea namna shughuli mbalimbali zinavyofanyika mjengoni humo.
Steve Gannon akitazama picha za wasanii mbalimbali wa nje waliowahi kufika nchini Tanzania na kufanya maonesho yao kadhaa ndani ya ofisi za Prime Time Promotions Ltd.


Mkurugenzi wa mambo ya utafiti na vipindi vya Clouds Media Group,Ruge Mutahaba akifafanua jambo kwa Mkurungezi Mtendaji wa Kampuni ya bia ya Serengeti,Steve Gannon ambaye nae alikuwa akimsikiliza kwa makini.
Mkurungezi Mtendaji wa Kampuni ya bia ya Serengeti,Steve Gannon akimuuliza jambo mtangazaji wa kipindi cha Power Breakfast,Gerald Hando kuhusiana na mambo mbalimbali ya kikazi,alipotembezwa kwenye studio ya ziada.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Clouds Media Group,Joseph Kusaga 'Joe' pichani kushoto akifafanua jambo kwa Mkurungezi Mtendaji wa Kampuni ya bia ya Serengeti,Steve Gannon mara baada ya kufanya ziara fupi mwishoni mwa wiki na kutembelea vitengo vyote kampuni hiyo huku akijionea namna shughuli mbalimbali zikifanya mjengoni humo.

Mkurungezi Mtendaji wa Kampuni ya bia ya Serengeti,Steve Gannon akizungumza jambo na baadhi ya wafanyakazi wa kitengo muhimu cha kampuni hiyo cha Masoko.
Steve Gannon akisalimiana na Oparesheni Meneja wa Prime Time Promotions Ltd.Balozi Kindamba,mara alipotembelea ndani ya kampuni hiyo ambayo imekuwa ikijihusisha na matamasha mbalimbali likiwemo tamasha kubwa la Fiesta ambalo hufanyika kila mwaka.
Steve Gannon akisalimiana na Gerald Hando
Mkurungezi Mtendaji wa Kampuni ya bia ya Serengeti,Steve Gannon akioneshwa matoleo mbalimbali ya jariba la burudani la KITANGOMA linachapishwa na kampuni ya Prime Time Promotions.


Mkurungezi Mtendaji wa Kampuni ya bia ya Serengeti,Steve Gannon akipeana mkono na Mmoja wa wafanyakazi wa Prime Time Promotions,Godliva Nicholaus mara alipowasili ndani ya ofisi za kampuni hiyo.
Mkurugenzi wa mambo ya Masoko na Mauzo,Shebba Kusaga akifafanua jambo kwa Mkurungezi Mtendaji wa Kampuni ya bia ya Serengeti,Steve Gannon.
Chief Editor wa Clouds TV,Bwa.Kanyopa akitoa maelezo mafupi kuhusiana na ufanyaji wao kazi ikiwemo na urushaji wa vipi kupitia Tv yao,Pichani kushoto ni Boss Joe akisikiliza kwa makini.


Mkurungezi Mtendaji wa Kampuni ya bia ya Serengeti,Steve Gannon alitembezwa pia ndani ya chumba maalum cha kuandalia habari,hapa Mtangazaji wa kipindi cha Michezo Shaffih Dauda akifafanua jambo kwa Steve Gannon.
Baada ya ziara kutembelea vitengo mbalimbali vya kampuni hiyo,pia Steve Gannon alipata wasaa wa kukaa meza moja na uongozi wa juu wa kampuni hiyo na kuzungumza machache,ikiwa ni sehemu ya mchakato wa ufanisi wa kikazi kwa mwaka mpya wa 2013. 

ALAMA YA BARABARANI HAIELEWEKI AU NDIO MAKUSUDI

Malori yakiwa yameegeshwa ndani ya hifadhi ya barabara ya mandela karibu na kituo Cha Gereji Huku kibao Cha Alama za Barabarani ambcho kinaonyesha alama ya kutokurusu Kuegesha Kikiwa Pembeni ya malori hayo. Je hii ni dharau au mwenye malori hayo yupo Juu ya Sheria au yupo sahihi kwa kuegesha magari yake hapo?

BALOZI WA NIGERIA NCHINI MAREKANI AMFANYIA DINNER YA KUMUAGA BALOZI WETU MH. MWANAID MAAJAR


Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico Mhe. Mwanaidi Maajar (wapili toka kulia)akiingia nyumbani kwa Balozi wa Nigeria (hayupo pichani) Potomac, Maryland, huku wakipokelewa na afisa ubalozi wa Nigeria (wa kwanza kulia) anayesalimia ni mama Lily Munanka ambaye ni mkuu wa utawala na fedha Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani akifuatiwa na mume wa Balozi, Bwn. Shariff Maajar siku ya Jumapili January 6, 2013 siku Balozi wa Nigeria alipomfanyia chakula cha jioni maalum kwa ajili ya kumuaga Balozi wetu ambaye anamaliza muda wake.
Mhe. Mwanaidi Maajar akilakiwa na Balozi wa Nigeria nchini Marekani, Mhe.Adebowale Ibidpo Adefuye siku ya Jumapili January 6, 2013 alipomkaribisha chakula cha jioni maalum kwa ajili ya kumuaga Balozi wa Tanzania nchini Marekani ambaye anamaliza muda wake.
Mke wa Balozi wa Nigeria akisalimiana na kumkaribisha Mhe. Mwanaidi Maajar huku mumewe Bwn. Shariff Maajar akiwa amesimama kwenye ngazi akiangalia.
Balozi na mumewe Bwn. Shariff Maajar wakisalimiana na Rais wa Jumuiya ya Watanzania DMV, Bwn Idd Sandaly ambaye pia aliongozana na mkewe (wakwanza kushoto) kwenye chakula cha jioni alichoandaliwa Balozi wetu na Balozi wa Nigeria kwa ajili ya kumuaga siku ya Jumapili January 6, 2013 nyumbani kwake Potomac, Maryland.
Kutoka kushoo ni Rais wa Jumuiya ya Watanzania DMV akiwa pamoja na mkewe, Balozi wa Benin nchini Marekani Mhe.Cyrille S. Oguin katika picha ya pamoja na Balozi wa Nigeria nchini Marekani Mhe.Adebowale Ibidpo Adefuye.
Balozi wa Nigeria nchini Marekani Mhe.Adebowale Ibidpo Adefuye (kulia) akisalimiana na Mume wa Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico, Bwn. Shariff Maajar.
Balozi wa Nigeria nchini Marekani Mhe.Adebowale Ibidpo Adefuye akisalimiana na kumkaribisha Balozi wa Botswana nchini Marekani Mhe. Tebelelo Seretse nyumbani kwake Potomac, Maryland siku ya Jumapili January 6, 2013 alipomualika chakula cha jioni maalum kwa ajili ya kumuaga Balozi wetu ambaye anamaliza muda wake.
Balozi wa Botswana nchini Marekani Mhe. Tebelelo Seretse (kushoto) akiongea jambo na Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico, Mhe. Mwanaidi Maajar.
Kutoka kushoto ni Mkuu wa Utawala na Fedha Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico, mama Lily Munanka, Mke wa Balozi wa Zimbabwe, Balozi wa Zimbabwe nchini Marekani, Mhe. Dr. Machivenyika Mapuranga na Balozi wa Benin nchini Marekani Mhe. Cyrille S. Oguin.
Wakati wa chakula.Picha na Vijimambo Blog

No comments:

Post a Comment