Thursday, November 29, 2012

WAZIRI KUU MIZENGO PINDA AZINDUA MPANGO WA KUTOKOMEZA MALARIA UNAOITWA “MALARIA SAFE


 
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Mh. Mizengo Pinda akizungumza na Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dk. Hussein Mwinyi wakati akiwasili kwenye hoteli ya Hyatt Regency Dar es Salaam kwa ajili ya kuzindua rasmi kampeni ya kupambana na Malaria inayoitwa “Malaria Safe Companys” ambapo Wizara ya afya inashirikiana na pamoja na taasisi za kimataifa na  Makampuni mbalimbali pamoja na Sekta ya michezo, ambapo wadau mbalimbali wameshiriki katika uzinduzi huo unaofanyika usiku huu jijini Dar es salaam, kulia ni Kaimu Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mh. Raymond Mushi.
 
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Mh. Mizengo Pinda akizungumza na Rais Washirikisho la Mpira wa miguu nchini TFF Bw. Leodger Tenga wakati alipowasili katika hoteli ya Hyatt Regency Dar es Salaam  kwa ajili ya uzinduzi wa kampeni ya kupambana na ugonjwa wa Malaria, kushoto ni Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dk. Hussein Mwinyi.
 
Wadau waliohudhuria katika uzinduzi wa kampeni ya kupambana na ugonjwa wa malaria kutoka kulia ni Mkurugenzi wa michezo katika Wizara ya Habari, Vijana , Michezo na Utamaduni Bw. Leonald Thadeo, Assah Mwmbene Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo, Mbunge wa Jimbo la Temeke Mh. Abbas Mtemvu na Mbunge na Waziri wa zamani Mh. Chrisant Mzindakaya.
 
Wadau mbalimbali wakiwa katika uzinduzi huo  katika Hyatt Regency Dar es Salaam
Mkurugenzi wa Sahara Media Bw. Samwel Nyala kushoto akiwa na wadau wengine katika uzinduzi huoHyatt Regency Dar es Salaam.
 
Wadau mbalimbali waliohudhuria katika uzinduzi huo kwenye hoteli ya Hyatt Regency Dar es Salaam
 
Waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda akiandika kitu huku Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Mh. Hussein Mwinyi akipiga makofi katika uzinduzi huo.
 
Meneja Mkuu wa Kampuni ya Azam Mzee Salim Mohamed Abeid Bakhressa akitoa ushuhuda kuhusu malaria ilivytokomezwa katika viwanda vyao.
 
Rais wa Shirikisho la mpira wa miguu nchini  TFF Bw, Leodger Tenga akizungumza katika hafla ya uzinduzi huo jinsi sekta ya michezo ilivyosaidia kutokomeza malaria nchini.
 
Mwimbaji nguli wa muziki wa Taarab Khadija Kopa pamoja na kundi lake wakitumbuiza katika hafla hiyo iliyofanyika usiku huu kwenye hoteli ya Hyatt Regency Dar es Salaam
 
Meneja Mkuu wa Bodi ya Utalii nchini Tanzania TTB Bw. Geofrey Meena akiwa katika hafla hiyo, Bodi ya Utalii nchini TTB ni moja ya taasisi zilizotambuliwa na Mh. Waziri Mkuu Mizengo Pinda katkatika hfla hiyo kwa juhudi zake za kupamana na ugonjwa wa malaria.

IKULU:VIONGOZI WAKUU WA NCHI WANACHAMA WA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI WAZINDUA JENGO LA MAKAO MAKUU YA JUMUIYA JIJINI ARUSHA


Mfano wa  jengo la Makao makuu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na viongozi wenzie wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wakiangalia mfano wa jengo jipya la makao makuu ya Jumuiya hiyo pamoja na maelezo yake baada ya kulifungua rasmi  Novemba 28, 2012 jijini Arusha
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na viongozi wenzie wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wakifunua pazia  kufungua rasmi jengo jipya la makao makuu ya Jumuiya  Novemba 28, 2012 jijini Arusha
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na viongozi wenzie wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wakikata utepe kufungua rasmi jengo jipya la makao makuu ya Jumuiya  Novemba 28, 2012 jijini Arusha
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na viongozi wenzie wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki  wakitembelea sehemu mbali mbali za jengo jipya la makao makuu ya Jumuiya  baada ya kulifungua rasmi Novemba 28, 2012 jijini Arusha
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na viongozi wenzie wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki  wakitembelea sehemu mbali mbali za jengo jipya la makao makuu ya Jumuiya  baada ya kulifungua rasmi Novemba 28, 2012 jijini Arusha. Hapa ni katika chumba cha mahakama ya jumuiya hiyo
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na viongozi wenzie wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki  wakishuhudia Mwenyekiti wa Jumuiya Rais Mwai Kibaki wa Kenya akizindua rasmi mfumo wa kisasa wa kuunganisha shughuli za ushuru wa forodha kwa njia ya mtandao katika  jengo jipya la makao makuu ya Jumuiya  baada ya kulifungua rasmi Novemba 28, 2012 jijini Arusha
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na viongozi wenzie wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki  wakiwa katika chemba ya mikutano ya Bunge la Jumuiya ya Afrika mashariki katika jengo jipya la makao makuu ya Jumuiya  baada ya kulifungua rasmi Novemba 28, 2012 jijini Arusha
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na wakuu wenzie wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wakiwa katika picha ya pamoja na wadau pamoja na wabunge wa Afrika Mashariki.Picha na IKULU

WADAU WA TAKWIMU NCHINI WAKUTANA KATIKA KONGAMANO LA PILI LA MWAKA JIJINI DAR LEO

 Mkurugenzi wa Takwimu nchini, Morrice Oyuke, akisoma hotuba yake kumwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa  TAKWIMU nchini Dkt.. Albina Chuwa, wakati wa kongamano la pili la mwaka la wadau wa TAKWIMU nchini lililofanyika leo jijini Dar es Salaam. 
 Mwakilishi kutoka Benki ya Dunia, Thomas Danielewitz, akitoa hotuba yake  leo jijini Dar es Salaam katika ufunguzi wa kongamano la pili la mwaka kwa  Wadau wa Takwimu nchini.  Kongamano hilo la siku moja limefunguliwa na Naibu Waziri wa Fedha Dkt. Saada M. Salum (hayupo Pichani).
 Baadhi ya washiriki  wa kongamano la pili  la mwaka unaowashirikisha  Wadau wa Takwimu nchini  wakimsikilza Naibu Waziri wa Fedha Dr. Saada M. Salum (hayupo pichani) katika ufunguzi wa kongamano hilo leo jijini Dar es Salaam.
 Naibu wa Wizara ya Fedha Dkt. Saada M. Salum akifungua kongamano la pili la mwaka kwa wadau wa Takwimu nchini leo jijini Dar es Salaam., ambapo amewasisitiza  wadau kutumia takwimu zilizo  sahihi. Picha na Mwanakombo Jumaa- MAELEZO

No comments:

Post a Comment