Monday, November 5, 2012

UBALOZI WA JAPAN KUTIA SAINI MSAADA WA SHILINGI MILIONI 380 ZA UJENZI WA BWENI LINDI NA SHULE YA WALEMAVU MTWARA


Balozi wa Japan Mr. Masaki Akodo
 
Balozi wa Japan nchini Tanzania, Masaki Okada kesho anataraji kutia saini makubalino ya msaada wa fedha kiasi cha shilingi Milioni 380 kwaajili ya miradi miwili ya ujenzi wa bweni La Wasichana pamoja na Shule ya watoto wenye ulemavu katika mikoa ya Lindi na Mtwara.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na Ubalozi huo jijini Dar es Salaam, inasemakuwa miradi hiyo ni upanuzi wa shule ya wenye ulemavu Dinyecha Wilayani Mtwara utakao gharimu zaidi ya shilingi Milioni 192 na ujenzi wa bweni la wasichana sekondari ya Ngapa ya Lindi utakaogharimu shilingi Milioni  188.

Miradi hiyo miwili inasimamiwa na taasisi za Tanzania Life Improvement  Association (TALIA) ya Mtwara na Women in Social Entrepreneurship (WISE) ya mjini Lindi.

Ubalozi wa Japan nchini Tanzania umekuwa ukichangia fedha katika miradi mbalimbali ya Maendeleo katika sekta ya Afya, elimu na maji tangu mwaka 1991 ambapo katika kipindi cha miaka 5 iliyopita mikoa ya Lindi na Mtwara imepatiwa msaada katika miradi 71 iliyogharimu dola za kimarekani 6,135,418 sawa na shilingi Bilioni 9,614,629485.

Utiaji saini huo utafanyika katika ofisi za mkuu wa Mkoa wa Lindi na Mtwara kati ya saa 3 asubuhi na saa 5.

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII ATEMBELEA BANDA LA TANZANIA KATIKA MAONYESHO YA UTALII YA WTM YANAYOFANYIKA JIJINI LONDON UINGEREZA

Waziri wa maliasili za Utalii Balozi Khamis Kagasheki akihojiwa na kituo cha Televisheni ya Taifa TBC mara baada ya kutembelea mabanda ya makampuni ya Tanzania yanayoshiriki katika maonyesho ya Utalii ya World Travel Market yanayoandaliwa na kufanyika katika eneo la Excell jijini London nchini Uingereza, yakishirikisha makampuni mbalimbali ya utalii kutoka pande zote za dunia, Mwaka huu Tanzania inawakilishwa na makampuni zaidi ya 55 yakiwa chini ya Bodi ya Utalii nchini Tanzania (TTB).
Waziri Balozi Kagasheki amesifushiriki wa makampuni ya Tanzania katika maonyesho hayo lakini amesisitiza kwamba makampuni hayo yaongeze juhudi za kutangaza utalii wa Tanzania mpaka kufikisha lengo la idadi ya watalii milioni moja kila mwaka, ameongeza kwamba kuna haja ya kuongeza vitanda zaidi nchini Tanzania ili kuongeza idadi ya watalii watakaotembelea katika mbuga zetu na kufanya utalii kuka zaidi, Maonyesho hayo yatazinduliwa rasmi kesho.
Fullshangweblo iko jijini London nchini Uingereza ikikumuvuzishia matukio haya moja kwa moja kutoka katika maeneo ya Excell ambako ndiko maonyesho hayo yanafanyika.
Waziri aliasili na Utalii wa Balozi Khamis Kagasheki akisalimiana na Issa Ahmed Othman Mshauri wa Rais masuala ya Utalii Zanzibar wakati alipotembelea banda la Tanzania katika maonyesho ya utalii ya (WTM) jijini London leo nchini Uingereza
Waziri Balozi Khamis Kagasheki akizungumza na Leila Ansel Mkuu wa mauzo na masoko kampuni ya Tanzania Zara Adventures wakati alipotembelea katika banda hilo leo kwenye maonyesho ya utalii ya WTM nchini Uingereza.
Yvone Baldwin Afisa mauzo wa kampuni ya ndege ya Precision Air akimkabidhi zawadi Balozi wa Tanzania nchini Uingereza Mh. Peter Kallaghe mara baada ya kutembelea banda hilo leo akiongozana na Waziri wa Maliasili Balozi Khamis Kagasheki.
Waziri wa Maliasili Balozi Khamis Kagasheki akizungumza na Rashid Adam Meneja Masoko wa Tanzania Zara Adventures wakati alipotembelea maonyesho ya Utalii ya WTM katika banda la Tanzania leo jijini London, wa pili kutoka kushoto ni Mh. Peter Kallaghe Balozi wa Tanzania nchini Uingereza na katikati ni mama Balozi.
Waziri Balozi Khamis Kagasheki akizungumza na Laura Meneja wa Maendeleo ya Biashara kampuni ya Laitolya Tours & Safari Ltd kushoto wakati alipotembelea banda la kampuni hiyo kwenye maonyesho ya WTM leo, kulia ni Mkurugenzi wa Masoko wa Bodi ya Utalii Tanzania TTB Devotha Mdachi.
Mkurugenzi wa Masoko wa Bodi ya Utalii Tanzania TTB Devotha Mdachi akiwahudumia watu mbalimbali waliotembelea katika banda la Tanzania leo katika maonyesho ya Utalii ya WTM jijini London Uingereza
Meneja Masoko wa Bodi ya Utalii ya Tanzania TTB Bw. Geofrey Meena akiwa katika picha ya pamoja na wakurugenzi wa African Environments Richard Beatty na Janice Beatty katika maonyesho hayo.
Leila Ansel Mkuu wa mauzo na masoko kampuni ya Tanzania Zara Adventures akizungumza na mmoja wa wageni waliotembelea katika banda la kampuni hiyo katikati ni Rashid Adam Meneja Masoko wa Tanzania Zara Adventures.
Mh. Peter Kallaghe Balozi wa Tanzania nchini Uingereza akizungumza na mdau Juma Mabakila wakati akitembelea banda la Tanzania kwenye maonyesho ya WTM
Meneja Masoko wa Bodi ya Utalii ya Tanzania TTB Bw. Geofrey Meena akiwasikiliza wageni mbalimbali waliofika katika banda la Tanzania katika maonyesho hayo leo.
Balozi Khamis Kagasheki Waziri wa Maliasili Utalii wa pili kutoka kulia akizungumza na Mkurugenzi wa Masoko wa Bodi ya Utalii Tanzania TTB Devotha Mdachi mara baada ya kutembelea Banda la Tanzania katika maonyesho ya Utalii ya WTM nchini Uingereza , kulia ni Mh. Peter Kallaghe Balozi wa Tanzania nchini Uingereza na katikati ni Mama Balozi.
Mmoja wa washiriki kutoka kampuni ya Africa Adventure akihojiwa na kituo cha televisheni cha TBC katika maonyesho ya Utalii ya WTM yanayofanyika jijini London nchini Uingereza.
Waziri Balozi Khamis Kagasheki akizungumza na wafanyakazi wa Mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro wakati alipotembelea maonesho hayo kushoto ni Meneja wa Masoko wa Bodi ya Utalii nchini TTB.
Washiriki mbalimbali wakiwa katika banda la Tanzania wakipokea wageni mbalimbali wanaotemelea kwenye banda hilo kwa ajili ya kupata taarifa mbalimbali kuhusu utalii wa Tanzania.PICHA NA FULLSHANGWEBLOG.COM

TIMU YA NMB FC YAKUBALI KICHAPO CHA MAGOLI 2 KWA 1 DHIDI YA EXIM FC


Mshambuliaji wa Exim FC, Erick Makule (kushoto) na mchezaji wa NMB F.C Omar Said (kulia) wakipigania mpira, katika mechi ya kirafiki iliyofanyika uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam jumapili jioni. Mechi ilimalizika kwa Exim F.C kuifunga NMB F.C 2-1. 
Mshambuliaji wa Exim FC, Ammy Ditufu (kulia) na mchezaji wa NMB F.C (kushoto) wakipigania mpira, katika mechi ya kirafiki iliyofanyika uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam Jumapili jioni. Mechi ilimalizika kwa Exim F.C kuifunga NMB F.C 2-1.
Na Mwandishi Wetu. 


TIMU ya mpira wa miguu ya benki ya Exim ya Tanzania, Exim F.C imeendeleza wimbi la ushindi katika michezo yake ya kirafiki, baada ya kuifunga timu ya NMB  magoli 2-1. 

Mchezo huo uliochezwa jana katika uwanja wa Karume ulianza kwa kasi hasa kutokana na timu hizo kuwa na upinzani mkubwa pale zinazopokutana.

Jambo hilo lilisababisha timu zote kuanza mchezo kwa kasi huku Exim ikionekana kuwa imara zaidi hasa kutokana na kusheheni wachezaji imara waliokuwa wanapeleka mashambulizi mara kwa mara langoni mwa NMB.

Dakika ya 5, NMB iliweza kupata goli la kwanza baada ya faulo iliyopigwa  na Aron Nyanda na kumkuta Nuhu Mkuchu.

Kuingia kwa goli hilo kuliamsha mashambulizi kwa timu ya Exim, ambayo ilifanya mabadiliko kwa kumtoa Richard Noni na kumuingiza Ami Ditufu.

Mabadiliko hayo yalionekana kuisaidia zaidi Exim, baada ya kuanza kulishambulia lango la NMB kama nyuki na kupelekea kukosa magoli ya wazi katika dakika ya 15, 17 na 20 kupitia kwa wachezaji wake Fadhili Selemani na Norbert Missana.

Kipindi cha pili kilipoanza, NMB walionekana kuzidiwa huku Exim ikindandaza kandanda safi na kuwasaidia kusawazisha goli kupitia kwa Ditufu.

Ditufu alishinda goli hilo, baada ya kupokea pasi safi ya  Missana na yeye kupiga shuti lililozaa goli hilo la kwanza kwa Exim.

Kuingia kwa goli hilo, kuliamsha ari ya ushindi kwa Exim  ambao walicheza vyema na kufanikiwa kufunga goli la pili kupitia kwa Missana.

Missana alishinda goli hilo katika dakika ya 57 na kuwafanya NMB kuzidi kupoteana na kuipa nafasi zaidi Exim kutawala mchezo huo. 

Hadi filimbi ya mwisho Exim ilifanikiwa kutoka uwanjani na ushindi huo wa magoli 2-1.

Akizungumza baada ya mchezo huo, nahodha wa Exim Fadhili Selemani alisema wanafurahi kuifunga NMB ambao ni wapinzani wao wakubwa.

“Hawa ni wapinzani wetu hivyo kuwafunga ni mwanzo tu, kwani tumejiandaa kuwafunga kila mechi hasa kutokana na kuwahi kutufunga michezo miwili”alisema.

Hivyo, alisema ushindi huo ni mwanzo kwa kuwa kila siku wanafanya mazoezi ya nguvu ili kuhakikisha wanashinda michezo yao yote.

Uzinduzi wa Mradi wa Miundombinu ya Gesi Asilia

RAIS KIKWETE AZINDUA MIRADI YA BARABARA MANYONI-ITIGI-CHAYA na ISSUNA-MANYONI MKOANI SINGIDA LEO


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikata utepe kufungua rasmi barabara ya Issuna-Manyoni akiwa na viongozi wa serikali na wa TANROADS pamoja na wabunge wa mkoa wa Singida.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akizindua ujenzi wa Barabara ya Manyoni-Itigi-Chaya mkoani Singida leo. Pembeni yake kulia ni Waziri wa Ujenzi Dkt John Pombe Magufuli.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipozi na viongozi wa serikali na wa kampuni ya ujenzi baada ya kuzindua ujenzi wa Barabara ya Manyoni-Itigi-Chaya mkoani Singida leo.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia wakati wa sherehe za uzinduzi wa ujenzi wa Barabara ya Manyoni-Itigi-Chaya mkoani Singida leo.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikata utepe kuzindua ujenzi wa Barabara ya Manyoni-Itigi-Chaya mkoani Singida leo.
Sehemu ya barabara mpya karibu na mji wa Manyoni iliyozinduliwa leo na Rais Kikwete.
Sehemu ya barabara mpya iliyozinduliwa na Rais Kikwete karibu na mji wa Katesh mkoani Manyara.
Sehemu ya barabara mpya iliyozinduliwa na Rais Kikwete mkoani Manyara. PICHA NA IKULU

JICHO LA LUKAZA BLOG LIKIANGAZIA MAENEO MBALIMBALI YA TABATA KINYEREZI JIONI HII

 Huo unaonekana kwenye picha ni Mbuyu, Mbuyu huo ndio umefanya eneo hilo linaloonekana kwenye picha kuitwa Mbuyuni eneo hilo lipo Tabata Kinyerezi Njia panda ya kuelekea majumba Sita.
 Ukiwa unatokea Segerea Kuelekea Kinyerezi lazima upite hapa
 Kijiwe Cha Bodaboda Kilichopo Kinyerezi Mwisho wa daladala

Tamasha la Kuchangia Mtoto wa Kike Nchini Uingereza

Mstahiki Meya akifungua Tamasha.
Mama Balozi akiwaonyesha wageni Rasmi Mameya vitu mbalimbali  vitakavyouzwa kwa ajili ya kuchangia mfuko huu.
Mtahiki Meya akiangalia sehemu ya chakula ya Tanzania.
kutoka Kushoto Mh balozi wa Grenada Ruth Elizabeth Rouse, Mtahiki Meya Christopher Buckmaster na Mama Balozi Joyce Kallaghe.
Mama Kiondo akiwa kikazi zaidi kuitangaza Tanzania Pics .
Mama Balozi Akipakwa Hina kwa ajili ya kuchangia Mfuko wa elimu
Mama Balozi akimkabidhi Mayorese Mrs. Anne Hobson baada ya kununua kitenge katika banda la Tanzania .
Mayorese Mrs. Anne Hobson katika banda la Tanzania.
wateja wakinunua bidhaa kutoka banda la Tanzania.
Sherehe ikiendeleaPics By Frank Eyembe.
Ukumbi wa Royal Borough of Kensington.Pics By Frank Eyembe.
---
Salaam,

Jumuiya ya Commonwealth Countries League (CCL) inayoshirikisha nchi hamsini na nne (54) duniani kutoka katika jumuiya ya madola iliandaa tamasha maalum siku ya jumamosi tarehe 3.11.12 kwa ajili ya kuchangia mfuko wa kumsaidia na kumwezesha msichana kusoma elimu ya sekondari.

Historia ya Commonwealth Countries League ilianzishwa rasmi kutoka kwa  baadhi ya wanawake mnamo mwaka 1923 nchini Australia kwa ajili ya kusaidia kutangaza uelewa wa haki sawa kati ya wanawake na wanaume waliopo nchi  mbalimbali zilizo ndani katika jamuiya  ya madola.

Tamasha hili  lilifanyika Royal Borough of Kensington chini ya uongozi kutoka kwa Mh. Balozi wa Grenada Ruth Elizabeth Rouse ambaye ndio raisi wa jumuiya hiyo akisaidia na makamu wake mama Balozi Joyce Kallaghe. Wageni Rasmi walikua  Wastahiki Mameya wa Worshipful  Royal Borough of Kensington na Chelsea - Councillor Christopher Buckmaster na  Mrs. Anne Hobson Shughuli ya mwaka huu iliandaliwa na wake za mabalozi kutoka katika jumuiya za Madola hamsini na nne (54) ili kuchangisha pesa kwa njia ya kuuza vitu mbalimbali vya asili kama chakula, urembo, maua, vinywaji n.k. Fedha zote zilizopatikana zilipelekwa kusaidia mfuko huu wa Elimu kwa ajili ya kumsomesha mtoto wa kike.

Aidha Mama Balozi Joyce Kallaghe aliongeza kwa kusema ''Elimu ni Ufunguo Wa Maisha kumsomesha mwanamke ni kuiwezesha jamii nzima hivyo vipaumbele vyote vimeelekezwa kwa kwa ajili ya kuwasomesha watoto wa kike walio maskini au wanaoishi katika mazingira magumu ambao wana uwezo wa kuendelea kusoma elimu ya sekondari katika nchi za jumuiya ya Madola". Tangu  mwaka 2011/2012 mfuko wa Elimu wa CCL ushawawezesha watoto wa kike 364 kutoka nchi 25  ikiwapo Tanzania. Pia aliwasihi wadau kuwa wazalendo kwa kuchangia mfuko huu kwa kuwasiliana kupitia barua pepe ccl.edfund@googlemail.com 

Kiasi cha paundi mia moja hamsini (£150) na Mia nne na hamsini (£450) zinatosha kumsomesha msichana kwa mwaka mzima

Asanteni

Urban Pulse Creative

KHADIJA KOPA ALIVYOFUNIKA MITIKISIKO YA PWANI DAR LIVE

Mzee Yusuf akimchombeza mkewe, Leila Rashid.
Mashabiki waliopanda stejini kumtunza Mzee Yusuf wakijiachia kwa raha zao.
Malkia wa mipasho nchini, Khadija Kopa, kutoka T.O.T akiwapagawisha mashabiki waliohudhuria Mitikisiko ya Pwani Dar Live Jumamosi.
Khadija Kopa na vijana wake wakiwa wameiteka Dar Live kwa burudani.
Kiongozi wa Kundi la Jahazi Modern Taarab, Mzee Yusuf 'Mfalme', akiimba na mashabiki wake.
Mke wa Mfalme, Leila Rashid, akilipamba Tamasha la Mitikisiko ya Pwani ndani ya Dar Live.
Mwanahawa Ally wa East African Melody akiwarusha mashabiki wa Mitikisiko ya Pwani.
Kiongozi wa kundi la Mashauzi Classic, Isha Ramadhan 'Isha Mashauzi', akiwapa raha mashabiki.
Maua Tego wa Coastal Modern Taarab akiwa stejini.
Sehemu ya mashabiki waliofurika Dar Live kushuhudia tamasha hilo.
Khadija Kopa na wasanii wenzake wa TOT wakilitawala jukwaa.
Wasanii wa TOT wakizidi kunogesha tamasha hilo.
Mashabiki wa Arsenal nao walikuwepo.
Wapenzi wa taarab waliokuwa VIP wakifuatilia tamasha hilo.
Isha Mashauzi akionyesha mbwembwe zake stejini.
Nyomi iliyohudhuria Tamasha la Mitikisiko ya Pwani.PICHA ZOTE NA RICHARD BUKOS / GPL
--
MALKIA wa mipasho nchini, Khadija Kopa, juzi (Jumamosi) alifunika vilivyo katika Tamasha la Mitikisiko ya Pwani lililofanyika ndani ya ukumbi wa kisasa wa Dar Live uliopo Mbagala Zakhem jijini Dar.

Tamasha hilo lilipambwa na makundi mbalimbali ya taarab yakiwemo Jahazi, Coastal, TOT na mengineyo. Watangazaji mahiri kutoka Times Radio wakiongozwa na Gardner G Habash na Khadija Shaibu 'Dida' walinogesha tamasha hilo na kulifanya liwe la kipekee.

No comments:

Post a Comment