Monday, October 15, 2012

Mkutano Wa Tathmini Wafanyika Leo

Shindano la kumtafuta mama Shujaa wa Chakula 2012 kufanyika leo

MAKAMU WA RAIS DKT GHARIB BILAL AFUNGUA MKUTANO WA KWANZA WA KIMATAIFA KATIKA BARA LA AFRIKA, WENYE LENGO LA KUTANGAZA UTALII WA NCHI ZA AFRIKA.

RAIS KIKWETE AWASILI MUSCAT OMAN KWA ZIARA YA SIKU 3

CHAMA CHA WAKUTUBI KUTOKA FINLAND(FLA) CHATOA MAFUNZO YA ICT KWA WAKUTUBI NCHINI

ALHAJI SHABAN MINTANGA AACHIWA HURU

"WOMEN IN BALANCE KITCHEN PARTY GALA" KUFANYIKA OKTOBA 21 MWAKA HUU DIAMOND JUBILEE VIP HALL.

MAMIA WAJITOKEZA KUUAGA MWILI WA KAMANDA LIBERATUS BALLOW LEO KATIKA UWANJA WA NYAMAGANA JIJINI MWANZA.

 Afande George Msangi akiongoza ratiba za kumuaga aliyekuwa kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza SACP Liberatus Ballow aliyeuawa usiku wa kuamkia jumamosi na watu wanaodhaniwa kuwa majambazi katika eneo la Kitangiri karibu na Hotel ya Tai Five.
 Msafara wa magari ya kuleta mwili wa marehemu Liberatus Ballow yakiingia katika uwanja wa Nyamagana ili viongozi na wananchi mbalimbali wapate kuuaga mwili huo.
                                       Magari yakiingia kwa uwanja wa Nyamagana..
 Maaskari walioteuliwa kubeba mwili wa marehemu Liberatus Ballow wakiwa wamejipanga vyema ili mwili uweze kutolewa ndani ya gari ili uwekwe sehemu nzuri ambayo kila mtu anaweza kuuaga vizuri.
                                     Hapa wakiushusha kutoka ndani ya gari ili waweze kuubeba.
            Safari ya kuelekea sehemu maalum iliyopangwa kwa ajili ya mwili wa marehemu ilianza hiviii..
                                          Maaskari wakiwa sawa kutekeleza jukumu lao..
 Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Injinia Everest Ndikillo akienda kuuaga mwili wa marehemu kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza Liberatus Ballow katika uwanja wa Nyamagana leo.
 Viongozi mbalimbali wa Kiserikali wakisimama kwa dakika chache kuupa heshima mwili wa marehemu kamanda Liberatus Ballow.
             Baadhi ya Maafisa wa Jeshi la Polisi wakionekana na huzuni
                Afisa Usalama wa Taifa Meja Jacob Mutashi mwenye suti nyeusi kulia akionekana pichani.
                     Mwili wa Marehemu kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza Liberatus Ballow.
 Mwandishi Peter Fabian kutoka gazeti la Mtanzania akiweka picha vizuri ya marehemu kamanda Liberatus Ballow.
 Saluti kutoka kwa Maafisa wa Polisi walizamu kwa Marehemu Kamanda wa Mkoa wa Mwanza Liberatus Ballow wakitoa heshima za mwisho.
 Katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza Joyce Masunga akiweka saini katika daftari la maombolezo katika msiba wa marehemu kamanda Liberatus Ballow katika uwanja wa Nyamagana.
 Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai Kaminishina Richard Manumba akisalimia na Mkuu wa Wilaya ya Magu Bi. Jackline Wana huku Katibu tawala wa Mkoa wa Mwanza Bi. Rosemary Mwanyika akiwa mbele mwenye suti nyeusi.
 Ibada ya ya kumuaga mwili wa marehemu kamanda Liberatus Ballow kama ilivyoongoza na Watumishi wa Kanisa la Roman Katoliki maana kamanda alikuwa muumini wa kanisa hilo.
 Wakuu wa wilaya mbalimbali katika Mkoa wa Mwanza na baadhi ya viongozi wa serikali, vyama vya kisiasa wakionekana katika picha wakiwa na majonzi makubwa kumpoteza kamanda Liberatus Ballow.
 Wananchi mbalimbali kutoka katika Mkoa wa Mwanza na nje ya Mkoa wa Mwanza wakionekana katika tukio la kuuaga mwili wa Kamanda Liberatus Ballow.
 Wanafamilia wa marehemu kamanda Liberatus Ballow wakiwa na majonzi makubwa sana katika uwanja wa Nyamagana wakati wa kuuaga mwili wa mpendwa wao Liberatus Ballow.
 Maafisa wa Majeshi aina mbalimbali kutoka Tanzania wakionekana katika hafla la kuuaga mwili wa marehemu kamanda Liberatus Ballow.
            Mabanda ambayo watu wamekaa kwa utulivu wakiuaga mwili wa kamanda Liberatus Ballow.
Umati mkubwa watu wakiwa katika uwanja wa Nyamagana wakati wa kuuaga mwili wa aliyekuwa kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza SACP Liberatus Ballow. Picha zote na B Plus Blog

No comments:

Post a Comment