Sunday, October 28, 2012

NMB YADHAMINI BONZA LA MICHEZO UDOM

RAIS KIKWETE AANZA ZIARA YA MKOA WA KILIMANJARO

GARI AINA YA HONDA IPO SOKONI

KIPANYA LEO....

Taswira:Cheki Jinsi Viongozi Wapya UVCCM Walivyopokelewa Kwa Mapigano Jijini Dar es Salaam

Zitto Kabwe:'' Tutaweka wazi majina ya Watanzania wenye akaunti Uswiss kwa utaratibu na umakini.Nitataja orodha hiyo Bungeni na kamwe sitataja nje ya Bunge. Hii ni kazi kubwa inahitaji utulivu.”

TAARIFA KWA UMMA KUTOKA WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII:TAHADHARI YA UGONJWA WA MARBURG

TAHADHARI YA UGONJWA WA MARBURG
Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, imepokea taarifa kutoka Shirika la Afya Duniani (WHO), tarehe 20 Oktoba, 2012 kuhusu ugonjwa wa Marburg ambao umejitokeza katika nchi jirani ya Uganda. Maeneo yaliyokumbwa na ugonjwa huo ni Wilaya ya Kabale, Kanda ya Kusini Magharibi ya nchi, na wilaya hii inapakana na Rwanda. Mpaka tarehe 24 Oktoba 2012, takriban watu 13 wamepata maambukizo na 6 wamepoteza maisha..

Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii inapenda kutoa tahadhari ya Ugonjwa huu kwa wananchi wote, katika mikoa yote ya Tanzania na hasa wale waliopo katika mikoa ambayo inapakana na na nchi jirani ya Uganda (Mikoa ya Mara, Mwanza, Kagera na Kigoma).

Marburg ni ugonjwa wa hatari unaofanana na Ebola na unasababishwa na virusi vijulikanavyo kwa lugha ya kitaalam “Marburg Virus”. Ugonjwa huu ni miongoni mwa magonjwa yajulikanayo kwa ujumla kama Homa za Virusi zinazosababisha kutokwa damu mwilini, (Viral Haemorrhagic Fevers). Chanzo kamili cha virusi vya ugonjwa huu hakijulikani. Hali inayosababisha mlipuko wake pia haijulikani. Ugonjwa huu hauna tiba wala chanjo.

Dalili kuu za ugonjwa huu ni pamoja na Homa kali, inayoambatana na kutokwa damu katika matundu yote ya mwili yaani pua, njia ya haja kubwa na ndogo, mdomoni, masikioni, machoni, hali inayopelekea kifo kwa muda mfupi.

 Kipindi cha kuonekana kwa dalili za ugonjwa ni kati ya siku 3 hadi 9 baada ya kupata maambukizi.

Ugonjwa huu unaenea kwa urahisi sana na haraka kutoka mtu mmoja hadi mtu mwingine iwapo mtu atakuwa karibu na mgonjwa na kugusana na mate, damu, mkojo, machozi, kamasi, maji maji mengine ya mwili, ikiwa ni pamoja na jasho au kumgusa  mtu aliyekufa kwa ugonjwa wa Marburg.Ugonjwa huu pia unaweza kuenezwa iwapo mtu atagusa nguo au mashuka ya mgonjwa wa Marburg.

Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, imechukua hatua zifuatazo katika kukabiliana na tishio la ugonjwa huu:

  • Kutoa taarifa ya tahadhari ya ugonjwa huu kupitia kwa Waganga Wakuu wote wa Mikoa na Wilaya. Aidha taarifa hii pia imejumuisha namna mgonjwa anavyoweza kutambuliwa (Ainisho la Ugonjwa),  “Fact sheet” ya ugonjwa, Mwongozo kwa watumishi wa afya wa namna ya kuchukua sampuli na vipeperushi vinavyoelezea ugonjwa huu.    
  • Kuimarisha ufuatiliaji wa ugonjwa huu kupitia kwa Wataalamu wa Afya katika Mikoa, Wilaya na maeneo ya mipaka. Aidha watalaamu hawa wa Afya pia wanatoa elimu kwa wananchi kuhusu dalili za ugonjwa huu ili endapo ugonjwa huo utatokea uweze kutolewa taarifa mapema.
  • Kupeleka vifaa kinga kwa ajili ya watumishi wa afya
Wananchi wanashauriwa kutokuwa na hofu kwani mpaka sasa hakuna mgonjwa yeyote aliyeripotiwa nchini. Wananchi wanashauriwa kutoa taarifa kwenye kituo cha huduma za afya kilicho karibu mara watakapoona mgonjwa yeyote atakayehisiwa kuwa na dalili za ugonjwa huu.

Kitengo cha mawasiliano ya Serikali
25/10/201

NAPE,MGEJA NA MAIGE WAFUNGA KAMPENI ZA CCM KATA YA BUGARAMA, KAHAMA

 Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akiwa katika mapokezi ya wananchi alipowasili kwenye mkutano wa kufunga kampeni za CCM za udiwani kata ya Bugarama, Kahama mkoani Shinyanga.
 Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akihutubia mamia ya wananchi katika mkutano wa kufunga kampeni za CCM za udiwani Kata ya Bugarama, Kahama mkoani Shinyanga, jana Oktoba 27.
 Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye Mbunge wa Msalala, Ezekiel Maige wakiwa na  watafiti wa madini  kutoka kampuni ya Majordrilling, katika kijiji cha Kakola wilayani Kahama mkoani Shinyanga.
 Baadhi ya Wazee wakifuatilia kwa makini hotuba ya Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye alipohutubia mkutano wa kufunga kampeni za udiwani za CCM  Kata ya Bugarama, Kahama mkoani Shinyanga. 
 Kina mama wakifuatilia kwa makini hotuba ya Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, Kata ya Bugarama , Kahama mkoani shinyanga.
 Mzee wa miaka 98, Nickson Toma akifuatilia kwa makini mkutano wa kampeni za udiwani Kata ya Bugarama mkoani Shinyanga uliohutubiwa na Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye.
 Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akicharaza ngoma kwenye mkutano wa kampeni za udiwani Kata ya Bugarama, Kahama mkoani Shinyanga.
 Wananchi katika kata ya Bugarama , Kahama mkoani Shinyanga, wakishangilia wakati wa kufunga kampeni za CCM za uchaguzi mdogo wa udiwani katika kata hiyo.
 Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akisalimiana kwa furaha na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Shinyanga Hamis Mgeja walipokutana katika Kata ya Kakola, kabla ya kwenda kwenye mkutano wa kufunga kampeni za udiwani za CCM kata ya Bugarama mkoani humo.
 Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Sinyanga Hamis Mgeja wakishiriki kucheza ngoma ya Baswezi kwenye mkutano wa kampeni za udiwani kata ya Bugarama mkoani humo.
 Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Sinyanga Hamis Mgeja wakishiriki kucheza ngoma ya Baswezi kwenye mkutano wa kampeni za udiwani kata ya Bugarama mkoani humo.
 Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akimsikiliza kwa makini Mbunge wa Msalala,  Ezekiel Maige wakati akimuombea kura mgombea udiwani wa CCM Kata ya Bugarama, kwenye mkutano wa kufunga kampeni za CCM uliofanyika mji mdogo wa Bugarama.
Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akimnadi mgombea wa Udiwani kata ya Bugarama, Nixon Igogo kwenye mkutano wa kufunga kampeni za udiwani za CCM.

USHABIKI KAZI DU...

Picha Kutoka

MABINGWA WA BALIMI BOAT RACE KAGERA WAPATIKANA

No comments:

Post a Comment