Sunday, May 20, 2012

Mwanzilishi na Mmiliki wa Mtandao Wa Facebook Mark Zuckerberg WENT FROM SINGLE TO MARRIED

Wed: Mark Zuckerberg and Priscilla Chan
Mark Zuckerberg and Priscilla Chan have married in a surprise ceremony in Palo Alto
Married: The couple have been together for nine years, but did not reveal their engagement
The couple have been together for nine years, but did not reveal their engagement
Arrival: Guests were pictured turning up at the Palo Alto home on Saturday afternoon
Guests were pictured turning up at the Palo Alto home on Saturday afternoon
 
Facebook founder and CEO Mark Zuckerberg updated his status to 'married' on Saturday afternoon. 
 
Food was served family-style and included dishes from the couple's favorite Palo Alto sushi restaurant. The two had been planning the marriage for months but were waiting until Chan had graduated to hold the wedding, the guest said.
 
The timing wasn't tied to the IPO, since the date the company planned to go public was a "moving target," the guest said. Even after the IPO, Zuckerberg remains Facebook's single largest shareholder, with 503.6 million shares. And he controls the company with 56 percent of its voting stock. Rather than his trademark hoodie, Zuckerberg wore a suit for the ceremony, while his bride wore a traditional wedding dress.
 
Zuckerberg and 27-year-old Priscilla Chan tied the knot at a small ceremony at his Palo Alto, Calif., home, capping a busy week for the couple, according to a guest authorized to speak for the couple. The person spoke only on the condition of anonymity.

Zuckerberg took his company public in one of the most anticipated stock offerings in Wall Street history Friday. And Chan graduated from medical school at the University of California, San Francisco, on Monday, the same day Zuckerberg turned 28, the person said.

The couple met at Harvard and have been together for more than nine years, the person said.
Zuckerberg designed the ring featuring "a very simple ruby," according to the person.

The ceremony took place in Zuckerberg's backyard before fewer than 100 guests, including Facebook's chief operating officer Sheryl Sandberg.

The guests all thought they were coming to celebrate Chan's graduation but were told after they arrived that the event was in fact a wedding.
"Everybody was shocked," the guest said.
The site, which was born in a dorm room eight years ago, has grown into a worldwide network of almost a billion people.

Zuckerberg founded Facebook at Harvard in 2004.He was selected as Time's Person of the Year in 2010, at age 26. Zuckerberg grew up in Dobbs Ferry, N.Y.

Rais Kikwete apata chakula cha jioni na uongozi wa Jumuiya ya Watanzania DMV


Rais Jakaya Mrisho Kikwete usiku wa kuamkia leo May 20, 2012 alikaribisha kwa chakula cha jioni uongozi wa Jumuiya ya Watanzania wanaoishi Washington na vitongoji vyake katika hoteli ya Ritz-Carlton jijini Washington DC. Uongozi huo, kwa niaba ya wanachama wake, ulimpongeza Rais Kikwete kwa kuwa mmoja wa Marais wanne wa Afrika walioalikwa kwa mara ya kwanza katika historia kuhudhuria kikao cha nchi tajiri duniani zijulikanazo kama G-8 katika makazi ya mapumziko ya Rais wa Marekani ya Camp David, Maryland. Rais wa jumuiya hiyo Bw. Iddy Sandaly alisema kwamba mualiko wa kuhuduhuria mkutano wa G-8 alioupata Rais Kikwete umeendelea kudhihirisha kwamba mataifa makubwa yanaheshimu msimamo wake katika kuendeleza kilimo cha kisasa na kuondoa njaa duniani, ambavyo ndivyo vilivyokuwa kauli mbiu ya mkutano wa Camp David.
 Hafla hiyo pia ilihudhuriwa na waziri wa kilimo Injinia Christopher Chiza pamoja na Waziri wa kilimo wa Zanzibar Mh Suleiman Othman Nyanga, pamoja na balozi wa Tanzania nchini Marekani Mh Mwanaidi Sinare Maajar. (Picha na Ikulu)

WAZEE WA YANGA WAMCHOMOA MWENYEKITI LOYD NCHUNGA MADARAKANI

Mwenyekiti wa Kamati ya Wazee wa Klabu ya Yanga, Ibrahim Akilimali akitangaza kumfuta Uenyekiti wa timu hiyo, Lyod Nchunga, baada ya kutimiza kolamu  ya wanachama mia tano na hamsini na sita na wajumbe nane kujiuzuru rasmi leo wakati wa mkutano wa wanachamauliofanyika kwenye klabu hiyo, Mtaa wa Jangwani naTwiga jijini Dar es Salaam.
Wanachama wa Yanga wakishangilia tamko la kumg'oa Mwenyekiti wa Klabu hiyo Lyod Nchunga
 Mashabiki wa Yanga ambao si wanachama, wakifuatilia mkutano wakiwa mbali
 Mmoja wa wanachama wa Yanga, anayeitwa Nyachia akionyesha kadi yake wakati wa kujisajili kuingia kwenye mkutano huo. Picha zote na Nkoromo Daily Blog: Fuatilia katika Blogu hii baadaye tunapandisha Video ya sehemu ya mkutano huo.
Tofauti na vikao vingine vya Yanga ambavyo hufanyika katika ukumbi wa  jengo la Klabu hiyo, mkutano huu wa leo unafanyika kwenye Uwanja nje ya jengo.( Picha kwa hisani ya http://bashir-nkoromo.blogspot.com/)

 

FLAVIANA MATATA KUTOA MSAADA KUMBUKUMBU YA MV BUKOBA

Mwanamitindo wa kimataifa Flaviana Matata Amekuja nchini akitokea nchini Marekani ambako ndiko yaliko makazi yake  kwa sasa mahsusi kwa ya ajili ya kugawa msaada wa  VIFAA VYA KUOKOLEA MAISHA MAJINI (life vest)  ikiwa ni miaka 16 tangu meli ya MV BUKOBA izame ambapo mama yake mzazi alifariki kwenye ajali hiyo
 
anatarajia kugawa msaada wa vifaa hivyo  Jumatatu ya 21 May  jijini mwanza

 

Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda Apongeza Uhusiona Uliopo Kati Japan na Tanzania,Ahaidi Kuimarisha Uhusiano wa Kibunge

Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda akimshukuru mwenyeji wake Spika wa Bunge la Japan Mhe. Takahiro Yokomichi na Ujumbe wake wa Wabunge wanaounda kamati inayoshughulikia Maswala ya Afrika kwa mwaliko waliompatia yeye na Ujumbe wa wabunge Kutoka Bunge la Tanzania kuja Japan kubadilishana uzoefu katika maswala ya Kibunge pamoja na kuimarisha ushirikiano kati ya mabunge haya mawili.  Kulia kwa Mhe. Makinda ni Mhe. Godfrey Zambi na Mhe. James Lembeli walioambatana Na Mhe. Spika katika Ziara hiyo. Picha na Owen Mwandumbya
--   
Na Mwandishi wetu, Tokyo Japan
Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda amesema, Tanzania inajivunia uhusiano mzuri kati yake na Japan. Akizungumza katika majumuisho ya ziara yake nchini Japan, Mhe. Makinda amesema, Bunge la Tanzania linaishukuru Serikali ya Japan na Bunge lake kwa kumwalika yeye na Ujumbe wa Wabunge kutoka Tanzania kuja kujifunza maswala Mabalimbali ya Kibunge ikiwa ni pamoja na kukuza demokrasia ya kibunge baina ya nchi hizi Mbili.
Amesema, Pamoja na Japan kupitia katika hali ngumu ya kulipuliwa kwa miji yake miwili ya Hiroshima na Nagasaki wakati wa Vita kuu ya Pili ya Dunia, Matetemeko ya mara kwa mara na mafuriko ya Tsunami, lakaini bado uchumi wake haujayumba kiasi kwamba sasa waJapan wameweza kusima imara kuijenga nchi yao.
Mhe. Makinda amesema Demokrasia safi  na Siasa imara za Japan ni mfano tosha na fundisho kwa Tanzania  ambapo hivi sasa katika kuimarisha uhusiano huu wa Kibunge, mabunge haya mawili yatabadilishana uzoefu katika maeneo mbalimbali kwa lengo la kuimarisha utendaji kazi wa Bunge la Tanzania. 
“ Nchini yenu mmekomaa sana katika Demokrasia,  ikiwa ni pamoja na  uendeshaji wa shughuli za Kibunge, sisi kama watanzania tuna mengi sana tungependa kujifunza kutoka kwenu, leo mmenialika na ujumbe wangu kutembelea Bunge lenu, lakini napenda kusema huu uwe ndio mwanzo wa kuimarisha uhusiano wetu, ikiwezekana hata kamati zetu za Bunge zipate fursa ya kujifunza kutoka kwenu. Ziara za namna hii zitatusaidia kupanua uelewa wetu katika maswala ya Kibunge“ alisema Mhe. Makinda.
Katika kuhakikisha kuwa Bunge la Tanzania linaimarisha uhusiano wake na Bunge la Japan, Spika Makinda ametoa Mwaliko maalum kwa Spika wa Bunge la Japan Mhe. Takahiro Yokomichi kuja kutembelea Tanzania ikiwa ni pamoja na kubadilishana uzoefu na wabunge wengine kutoka Bunge la Tanzania.
Mhe. Makinda amesema, Bunge la Tanzania linayo kamati ya Bunge inayoshughulikia maswala ya mambo ya Nje na uhusiano wa Kimataifa, hivyo ni fursa pekee ya kamati hii na wenzao kutoka Bunge la japan kushrikiana kwa karibu kuhakikisha ushirikano huu unakuwa imara na endelevu.
Akimshukuru Mhe. Makinda kwa kukubali mwaliko wake, Spika wa Bunge la Japan Mhe. Takahiro Yokomichi, amesema nchi yake iliichagua Tanzania miongoni mwa nchi za Afrika hususani Africa Mashariki kutembelea Bunge la Japan kwa kuwa ni nchi yenye demokrasia safi na siasa zake zinaimarika kila kukich na kuifanya Japan kuvutiwa na maendeleo hayo katika Bunge la Tanzania.
Mhe. Yokomichi amesema huu ni mwanzo wa ushirikiano muhimu baina ya Mabunge haya mawili ambapo Bunge la Japan pamoja na kuwa na kamati maalum inayoshughulikia maswala ya Afrika, bado kuna haja kwa kamati hiyo kufanya kazi kwa ukaribu na Bunge la Tanzania kwa lengo la kuangalia maeneo muhimu ambayo Japan itaisaidia Tanzania. 
 
Hata hivyo Mhe. Yokomichi ameaidi kuishawishi Serikali yake ya Japan ili iendelee kutenga fungu kubwa zaidi kwa lengo la kusaidia sekta mbalimbali za maendeleo nchini Tanzania. Tarari Japan ni mchangiaji Mkubwa katika sekta mbalimbali za maendelo kwa kiasi kikubwa.
 
Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda na Ujumbe wa wabunge  5 kutoka Bunge la Tanzania upo Japan kwa mwaliko maalum na Bunge la Japan kujadili na kuimarisha ushirikiano baina ya Mabunge haya mawili, ambapo kabla ya kuonana na Mwenyeji wake, Ujumbe huo wa Tanzania ulipata fursa ya kutembelea maeneo mbali mbali ya utalii nchi Japan ikiwa ni pamoja na eneo la Mji wa Natori lililokumbwa na mafuriko yaliotokea machi mwaka jana na Mji wa Hiroshima uliosambaratishwa na Bomu la Atomic wakati wa vita kuu ya dunia mwaka 1945. Spika na Ujumbe wake wanatarajia kurudi nchini jumanne wiki hii.
 
 
 
 

MISS EAST AFRICA 2012- UGANDA

              PRESS RELEASE                                                                                   
MISS EAST AFRICA 2012
Washiriki watakaoziwakilisha Nchi zao katika fainali mashindano ya Miss East Africa 2012 wanaendelea kutangazwa katika mchujo ulioendeshwa na kampuni ya East Africa gazelle ya Nchino humo.
Mrembo aliyetangazwa mwishoni mwa wiki ni  Miss Ayisha Nagudi (23)  kutoka Nchini Uganda atakayeiwakilisha Nchi hiyo katika fainali za mashindano ya Miss East Africa 2012.
Miss Ayisha Nagudi  ana urefu wa 1.82m ni mwanafunzi wa mwaka pili katika chuo kikuu cha Makelele jijini Kampala, ambapo anasomea degree ya Education
Fainali za mashindano ya Miss East Africa 2012 ambazo huandaliwa na kumilikiwa na Kampuni ya Rena Events Ltd, zitafanjika tarehe 07 mwezi September mwaka huu jijini Dar es salaam ambapo zitashirikisha Nchi za Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Somalia, Djibouti, Eritrea, Sudan, Ethiopia, Malawi, Madagascar, Reunion, Comoros, Seychelles, na Mauritius.

 

No comments:

Post a Comment