Saturday, May 26, 2012

TAASISI YA WANAFUNZI WANAOSOMA SHAHADA YA KWANZA YA SOSHOLOJIA YA CHUO KIKUU CHA DODOMA (UDOMSSO) YAPATA VIONGOZI WAPYA LEO MCHANA

Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Kutoka Mwaka wa 1 alipokua akitoa maelekezo ya nini kifanyike kabla ya Zoezi la Kupiga kura na Kutangaza washindi
 Mgombea wa Nafasi ya Mwenyekiti katika taasisi ya wanafunzi wanaosoma Shahada ya Kwanza ya Sosholojia ya Chuo Kikuu Cha Dodoma (UDOMSSO) Bw Edgar Kelvin ambaye anasomma mwaka wa 2 alipokua akinadi sera zake kabla zoezi la kupiga alijaanza
Mgombea wa pili wa nafasi ya Mwenyekiti katika taasisi ya Wanafunzi wanaosoma shahada ya kwanza ya Sosholojia ya Chuo Kikuu Cha Dodoma (UDOMSSO) Bi Loyce Haule ambaye anasoma mwaka wa 2 akinadi Sera zake
Mgombea wa Tatu wa Nafasi ya Mwenyekiti katika taasisi ya Wanafunzi wanaosoma shahada ya kwanza ya Sosholojia ya Chuo Kikuu Cha Dodoma (UDOMSSO) Bw Mwakindaga Emmanuel ambaye anasoma mwaka wa 2 akinadi sera zake
Mgombea Wa Nafasi ya Makamu Mwenyekiti katika taasisi ya Wanafunzi wanaosoma shahada ya kwanza ya Sosholojia ya Chuo Kikuu Cha Dodoma (UDOMSSO) Bw Mtono Juma ambaye amepita bila kupingwa kutoka na kuwa mgombea pekee wa nafasi hiyo na ni mwanafunzi kutoka mwaka wa kwanza
Mmoja wa Wanafunzi Kutoka Mwaka wa 3 Sophia Mkingiye akiuliza Maswala mara baada ya Wagombea kumaliza kunadi sera wakati walipokua wakiomba kura kwa wajumbe na wanachama
Mwanafunzi wa Mwaka wa 2 ambaye anasoma shahada ya kwanza ya Sosholojia ya Chuo Kikuu Cha Dodoma Bi Hadija Hassan alipokua akiuliza swali wakati kwa wagombea wa nafasi ya Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanafunzi wanaosoma shahada ya Kwanza ya Sosholojia ya Chuo Kikuu Cha Dodoma Wakati Wa Uchaguzi wa Kuwachagua Viongozi wapya wa Nafasi mbalimbali Katika Taasisi hiyo Mchana wa Leo
Baadhi ya wanafunzi wanaosoma Shahada ya Kwanza ya Sosholojia ya Chuo Kikuu Cha Dodoma waliohudhuria katika uchaguzi wa kuchagua viongozi wa taasisi ya Wanafunzi wanaosoma Shahada ya Kwanza ya Sosholojia ya Chuo Kikuu Cha Dodoma (UDOMSSO) katika uchaguzi uliofanyika ndani ya Chuo Kikuu Cha Dodoma mchana wa leo
Zoezi la Kuesabu kura likiendelea hapo 
Mwenyekiti aliyemaliza muda wake Bw Emmanuel Misungwi Alipokua akitoa Shukrani wa wanachama na wadau wa taasisi hiyo Kwa Kipindi Chote alichokua madarakani kwa mazuri na mabaya ambayo taasisi imepitia na kushukuru kwa wanachama kushiriki zoezi la kupiga kura na kupata viongozi wapya wa Taasisi ya Wanafunzi wanaosoma Shahada ya Kwanza ya Sosholojia ya Chuo Kikuu Cha Dodoma (UDOMSSO)
Baadhi ya Viongozi wapya wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi waliomaliza muda wao leo mara baada ya zoezi la kupiga kura kumalizika na hatimaye kuwapata viongozi wa taasisi ya wanafunzi wanasoma shahada ya kwanza ya Sosholojia ya Chuo Kikuu Cha Dodoma mchana wa leo
Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanafunzi wanaosoma Shahada ya Kwanza ya Sosholojia ya Chuo Kikuu Cha Dodoma aliyemaliza muda wake leo Mh Emmanuel Misungwi (Katikati) Akiwa katika Picha ya Pamoja na Mwenyekiti mpya wa Taasisi hiyo Mh Edgar Kelvin (Wa kwanza kulia) na Aliyekuwa Mwenyekiti Wa UChaguzi Wa Kwanza Kushoto


FINA REVOCATUS AIBUKA KIDEDEA NA KUWA REDD'S MISSS IFM 2012

Washiriki walioingia kwenye tano Bora.

Mshindi wa Redd's Miss IFM 2012,Fina Revocatus (katikati) akiwa na Mshindi wa Pili,Jane Augustino (kushoto) na wa Tatu Theresia Issaya muda mfupi baada ya kumalizika kwa shindano lao hilo lililofanyika usiku wa kuamkia leo kwenye ukumbi wa Hoteli ya Blue Peal,Ubungo Jijini Dar.

Msanii wa Muziki wa Bongo Fleva,Diamond akifanya vitu vyake wakati wa onyesho hilo la urembo  lililofanyika usiku wa kuamkia leo kwenye ukumbi wa Hoteli ya Blue Peal,Ubungo Jijini Dar.


RAIS KIKWETE KUFUNGUA MKUTANO WA AFDB AMBAO UTAGARIMU BILIONI 12

Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya mkutano wa (AFDB) Bw. Ngosha Magonya  katikati akiongea na waandishi wa habari mapema leo jijini Arusha.
Baadhi ya wanakamati wa kamati ya maandalizi ya mkutano wa AFDBwakiwa katika viwanja vya AICC jijini Arusha leo.

NA GLADNESS MUSHI WA FULLSHANGWE-ARUSHA
 Benki ya maendeleo ya Afrika (AFDB)inatarajia kutumia kiasi cha Shilingi bilioni 12 katika mkutano wake unaoanza Jumatatu jijini Arusha na kufunguliwa na Raisi Jakaya Kikwete  huku kiasi cha fedha hizo zikitumika kukarabati Kumbi mbalimbali za jengo la Kimaitaifa la ukumbi wa AICC kwa kuwa baadhi ya kumbi za jengo hilo zinaonekana kupitwa na wakati kutokana na utandawazi uliopo kwa sasa ndani ya nchi zilizoendelea
Akizungumza jijini hapa na waandishi wa habari mwenyekiti wa kamati ya kitaifa ya mkutano wa benki ya AFDB kwa mwaka 2012 Bw Ngosha  Magonya  ambapo alisema kuwa mkutano huo utakuwa na faida kubwa sana

Alifafanua kuwa kupitia mkutano huo ambao utaanza Jumatatu ijayo utakuwa na faida kubwa sana kwa jiji la Arusha kwa kuwa hata kiwango cha uchumi kitaaimarika sana kwa kuwa wageni mbalimbali kutoka katika maeneo ya nchi mbalimbali duniani watabadilishana hata uzoefu

“kwa kipindi hiki ambacho kuna mikutano ndani ya jiji la Arusha tunatarajia kuwepo na utoafuti wa khali ya juu sana hasa katika mchakato wa uchumi na kwa hali hii pia tunatarajia hata kufanya maendeleo mbalimbali  ikiwemo kufanya marekebisho kwa jengo la kimataifa la AICC”alisema bw Magonya

Katika hatua nyingine alifafanua kuwa mbali na kuweza kuimarisha uchumi wa mkoa wa Arusha pia wanatarajia kutumia fursa mbalimbali za kuhakikisha kuwa wanakutanisha wafanyabiashara mbalimbali huku malengo yakiwa ni kuendeleza uchumi kwa walengwa.

Pia alifafanua kuwa mbali na kuweza kuwasaidia wafanyabiashara hao katika michakato ya kukuza uchumi pia benki hiyo ina mikakati mbalimbali ya kuendeleza barabara ambazo zitaweza kutumika kama njia ya mawasiliano hapa Tanzania hali ambayo nayo itachangia kwa kiwango kikubwa sana hata kuimarisha uchumi wa nchi ya Tanzania

Aliongeza kuwa hapo awali benki hiyo ilikuwa imeshajenga barabara ya Arusha –Namanga kwa sasa ana mpango wa kujenga barabara ya Arusha – Holile ndani ya Mkoa wa Kilimanjaro hali ambayo itachangia sana maendeleo hasa ya mawasiliano

Alimalizia kwa kusema kuwa wafanyabiashara hasa wa mkoa wa Arusha wanatakiwa kuhakikisha kuwa wanatumia vema fursa za mkutano huo ili kuweza kuimarisha biashara zao za kila siku.
 
 

TAIFA KATIKA TASWIRA:Marais wastaafu wa Tanzania, Ali Hassan Mwinyi (kulia), Benjamin Mkapa (kushoto), Rais mstaafu wa Zanzibar, Amani Abeid Karume (katikati) sambamba na marais wengine wakiwasili kwenye Viwanja vya Chuo Kikuu cha Witwatersrand, Johannesburg, Afrika Kusini

 
Marais wastaafu wa Tanzania, Ali Hassan Mwinyi (kulia), Benjamin Mkapa (kushoto), Rais mstaafu wa Zanzibar, Amani Abeid Karume (katikati) sambamba na marais wengine wakiwasili kwenye Viwanja vya Chuo Kikuu cha Witwatersrand, Johannesburg, Afrika Kusini kwa ajili ya kuhudhuria Mkutano wa kujadili maendeleo ya matumizi ya nishati, Karne ya 21 kwa nchi za Afrika. (Na Mpigapicha Wetu).

WANAFUNZI WA CHUO CHA SAYANSI YA COMPUTA NA TEKNOLOGIA YA MAWASILIANO WAANZA KAMPENI ZA UCHAGUZI

hizi ndizo barabara za majengo ya hosteli za chuo hicho ambapo makundi ya watu mbalimbali hupita kwa kuimba nyimbo za harambee huku wakipiga kampeni
 baadhi ya kundi la mgombea wa urahisi akipita huku akiwapunga mkono wa salamu kwa wanafunzi waliokuwa wakimuangalia na kumshabikia
 msafara huu ulipambwa na nyimbo za kishujaa na mchakamchaka kwa mbaaaali
walihakikisha wanapita bweni baada ya bweni wakisaeeema mchague GEORGE kwani anafaa:habari picha na (ZE JOJO)

TAIFA KATIKA TASWIRA:MSHITAKIWA(John Mnyika) na MSHITAKI(Hawa Nghumbi) WAKIBADILISHANA MAWAZO MAHAKAMANI

Mbunge wa Ubungo kwa tiketi ya Chadema, John Mnyika(Kushoto) akiwa na aliyekuwa mgombea wa ubunge kwa tiketi ya CCM katika uchaguzi Mkuu 2010,Hawa Nghumbi, wakati wakisubiri hukumu, katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, kuhusu kesi  ya kupiga matokeo yaliyompa ushindi Mnyika iliyofunguliwa na Hawa Nghumbi kwenye mahakama hiyo.
 
 
 

Mwanamke Mkazi wa Rufiji Ajeruhiwa Mguu Alipokua Akipambana na Mamba

Mwanamke Mkazi wa Rufiji, Khadija Boma (40), kifanyiwa tiba na Muuguzi Geraidina Amani juzi katika wodi 2 ya Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI), Dar es Salaam, baada ya kujeruhiwa mguu alipokuwa akipambana na Mamba katika Mto Kipoka juzi, Rufiji. Mama huyo ambaye amekatwa mguu wa kulia aliong'atwa na Mamba, kabla ya kuokolewa na wananchi, alipambana naye huku akiwa na mtoto mgongoni.Picha na Khamis Mussa
 
 
 

 

TANZANIA BEGA KWA BEGA NA UNDP KUJENGA AFRIKA YENYE UHAKIKA WA CHAKULA.

 Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa UNDP nchini Tanzania Dk. Alberic Kacou akizungumza kwa niaba ya UNDP kuhusiana na kuzinduliwa kwa Ripoti ya Maendeleo ya Afrika 2012 ambapo amesema huu sasa ni wakati kwa nchi za Afrika haswa zilizo kusini mwa Jangwa la Sahara kujenga mazingira ya kuelekea mustakabali wenye uhakika wa chakula.
 Mshauri wa Uchumi UNDP Bw.Amarakoon Bandara akifanya 'presentation' ya Ripoti hiyo. Kushoto ni Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Dk. Alberic Kacou, Naibu Waziri wa Fedha Mh. Janet Mbene na Mkurugenzi wa UNDP Tanzania Bw. Phillipe Poinsot.
Mgeni rasmi Naibu Waziri wa Fedha Mh. Janet Mbene na Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa Tanzania, Dk. Alberic Kacou (kulia) wakifuatilia maoni ya Uchambuzi wa Ripoti ya Maendeleo ya Afrika 2012 kutoka kwa Maprofesa wa Vyuo vikuu nchini.
 Dr. John Mduma akifanya majumuisho ya nini kifanyike kukabiliana matatizo ya uhaba wa chakula yanayolikabili bara la Afrika na Afrika Mashariki.
Profesa Joyce Kinabo wa Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine akieleza uhifadhi wa Chakula kwa ajili ya matumizi ya baadae
Baadhi ya Maofisa wa Umoja wa Mataifa na Wadau wa Serikali wakichangia maoni yao kuhusiana na Ripoti hiyo.
 Mgeni rasmi Naibu Waziri wa Fedha Mh. Janet Membe (MB) akisoma hotuba wakati wa hafla ya Uzinduzi wa Ripoti ya Maendeleo ya Afrika 2012. Kushoto ni Mkurugenzi wa UNDP Tanzania Bw. Phillipe Poinsot.
Mgeni rasmi Naibu Waziri wa Fedha Mh. Janet Mbene (MB) akikata utepe kuzindua rasmi Ripoti ya Maendeleo ya Afrika 2012. Kushoto ni Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Dk. Alberic Kacou.
 "Sasa imezinduliwa rasmi" Mgeni rasmi Mh. Janet Mbene na Dk. Alberic Kacou wakionyesha Ripoti hiyo kwa wageni waalikwa na waandishi wa habari.
Baadhi ya Wageni waalikwa wakipitia Ripoti ya Maendeleo ya Afrika 2012 kuelekea kwenye Mustakabali wenye uhakika wa Chakula kwa nchi za Afrika iliyozinduliwa rasmi leo jijini Dar es Salaam

Bara la Afrika ikiwemo Tanzania limeshakumbwa na matukio kadhaa ya kukabiliwa na uhaba wa chakula, uliokwenda sambamba na matukio ya watu wengi kupoteza maisha haswa Kusini mwa jangwa la Sahara na Ukanda wa Sahel eneo la Afrika Magharibi.

Hali hiyo imekuwa moja ya changamoto kubwa inazozikabili serikali za mataifa hayo ambapo yanapambana ili kuitatua ili kila mwananchi barani Afrika aweze kufurahia kukua kwa uchumi.

Akitoa hotuba wakati akizindua rasmi Ripoti ya Maendeleo ya Afrika 2012 leo jijini Dar es Salaam, Naibu Waziri wa Fedha Mh. Janet Membe (MB) amesema kwa muda mrefu sura ya eneo la nchi za Afrika zilizo Kusini mwa jangwa la Sahara imekuwa ni ya njaa ya kukithiri, ambapo zaidi ya mtu mmoja katika kila waafrika wane wana tatizo la upungufu wa lishe.

Amesema Ripoti hiyo inaonyesha kuwa pamoja na ukweli kwamba baadhi ya nchi zinazokuwa kwa kasi kiuchumi katika kipindi cha miaka kumi ziko Afrika, lakini bado hali ya maisha ya waafrika ni duni.

Awali Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa UNDP nchini Tanzania Dk. Alberic Kacou alisema bara la Afrika limejaliwa kuwa na ardhi yenye rutuba, maji ya kutosha na hali nzuri ya hewa kwa kukuzia mazao, lakini swali la kujiuliza ni kwanini bado kuna uhaba wa chakula.

Hata hivyo Dk. Kacou ametoa matumaini kuwa bara la Afrika bado lina uwezo wa kujijengea mazingira ya kuwa na akiba ya kutosha ya chakula kwa kipindi kijacho.

Ripoti hii ya Kwanza ya Maendeleo ya Afrika inasema kwamba ongezeko endelevu katika uzalishaji kwenye kilimo kunalinda haki ya chakula na uwezo wa watu kupata chakula.
 

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL ASHIRIKI CHAKULA CHA JIONI KATIKA MKUTANO WA WAKUU WA NCHI ZA AFRIKA MJINI BOTSWANA

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal na Mama Asha Bilal, wakiwasili  kwenye ukumbi wa tafrija ya chakula cha jioni kilichoandaliwa na Rais wa Botswana Lt. General Seretse Khama, kwa viongozi wakuu wa Nchi za Afrika waliohudhuria mkutano wa siku mbili kuhusu maendeleo endelevu ya Bara la Afrika Nchini Gaborone Botswana, jana. 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal na mkewe Mama Asha Bilal, wakiwa kwenye tafrija iliyoandaliwa na Rais wa Botswana Lt. General Seretse Khama, kwa ajili ya viongozi wakuu wa Nchi za Afrika waliohudhuria mkutano kuhusu maendeleo endelevu kwa Bara la Afrika jana jioni.
 

Wasanii wa kikundi cha ngoma za utamaduni cha nchini Botswana wakitumbuiza kwenye hafla ya chkula cha jioni iliyoandaliwa maalum kwa wakuu wa nchi za Afrika waliohudhuria mkutano wa wakuu wa nchi za Afrika kuhusu maendeleo endelevu ya Bara la Afrikamjini Gaborone Botswana.

RAIS KIKWETE APOKEA UJUMBE MAALUM KUTOKA KWA RAIS ROBERT MUGABE WA ZIMBABWE

 Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, akipokea ujumbe maalum kutoka kwa Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe uliowasilishwa na Waziri wa nchi ofisi ya Rais Bwana, Sidney Sekeremayi, Ikulu ndogo mjini Dodoma leo asubuhi.

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika mazungumzo na Bwana Sidney Sekeremayi, ambaye ni mjumbe maalumu wa Rais Robert Mugabe Ikulu mjini Dodoma leo asubuhi. Picha na Freddy Maro
 
 
 

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad Akabidhi Bendera Ya Zanzibar Watoto Wanaowawakilisha Watoto Wenzao Mayatima Wakiwa na Viongozi Wao Wanaokwenda nchini Uturuki Kuiwakilisha Zanzibar

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akiwakabidhi bendera ya Zanzibar, Watoto wanaowawakilisha Watoto wezao Mayatima wakiwa na Viongozi wao wanaokwenda nchini Uturuki kuiwakilisha Zanzibar katika Kongamano la Kimataifa la Kuadhimisha Siku ya Watoto Yatima litakalofanyika mjini Istambul Uturuki kuanzia tarehe 28/05 hadi 03/06/2012. na kuwajumuisha Watoto wanaotoka  Nchi mbalimbali Nduniani kushiri katika Kongamano hilo.Picha na Salmin Said,-Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa  Rais Zanzibar
 
 

Waumini wa madhehebu ya Hindu kutoka Tanzania, Kenya, Afrika Kusini, Botswana, India na Uingereza wakiandamana kwenye mitaa mbalimbali ya Jiji la Arusha

Waumini wa madhehebu ya Hindu kutoka Tanzania, Kenya, Afrika Kusini, Botswana, India na Uingereza wakiandamana kwenye mitaa mbalimbali ya Jiji la Arusha kuashiria ufunguzi wa hekalu lao la Swaminarayan Mandir jana. (Picha na Marc Nkwame).
 

No comments:

Post a Comment