Thursday, June 21, 2012

Mkurugenzi Mkuu wa Mambo ya Nje wa Ufaransa Amtembelea Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP Dk. Reginald Mengi


Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP Dk. Reginald Mengi akifafanua jambo alipokutana na Mkurugenzi Mkuu wa Mambo ya Nje wa Ufaransa anayeshughulikia Ukanda wa Afrika na Bahari ya Hindi, Elisabeth Barbier  alipomtembelea Ofisini kwake kwa mazungumzo jijini Dar es Salaam


Taswira Za Mheshimiwa Godbless Lema Akiung'uruma Kwenye Mkutano Wa Hadhara Wa CHADEMA Manzese Jijini Dar es Salaam

 Aliyekua Mbunge wa Arusha Mjini(CHADEMA)Mheshimiwa Godbles Lema Akiunguruma leo kwenye mkututano wa hadhara Manzese jijini Dar es Salaam
Mwenyekiti wa Umoja wa Baraza la Vijana wa CHADEMA John Henche(kushoto)akifwatilia kwa makini mkutano wa Chadema Manzese leo
Mkuu wa  Kurugenzi ya Ulinzi na Usalama ya Chadema WilfredLwakatare(Kulia)akifwatilia kwa makini mkutano wa chadema leo
Sehemu ya Umati Mkubwa wa Wananchi waliojitokeza kwenye mkutano wa hadhara wa chadema Manzese jijini Dar es Salaam Leo.Picha na Kurugenzi Ya Habari-CHADEMA

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad Atembelea Chemchem ya Mtopepo Zanzibar

 Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maji Zanzibar (ZAWA) Dk. Mustafa Ali Garu, akimuonesha Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad namna chemchem inavyotiririka, katika chemchem ya Mtopepo walipofanya ziara ya kutembelea chemchem hiyo jana tarehe 19/06/2012.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad pamoja na uongozi wa ZAWA wakiangalia upungufu wa maji katika eneo la Mtopepo alipofanya ziara ya kutembelea chemchem ya Mtopepo jana. Kuliani kwake ni Waziri wa Ardhi, Makaazi, Maji na Nishati Mhe. Ramadhan Abdallah Shaaban.Picha na Salmin Said-Ofisi Ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar
---
 Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad amesema serikali italazimika kutumia ukali na kuondoa muhali kwa watu wanaoendeleza vitendo vya uchafuzi wa mazingira hasa katika vianzio vya maji. 

 Amesema ni hatari kuona vitendo hivyo vikiendelea huku taifa likikabiliwa na uhaba wa maji unaotokana na uharibifu wa mazingira katika vianzio hivyo. 
Akiwa katika ziara ya kutembelea vianzio vya maji katika chemchem ya Mtopepo, Maalim Seif ametahadharisha kuwa ikiwa vitendo hivyo vitaachiwa kuendelea, kuna hatari ya taifa kuwa na upungufu mkubwa wa maji katika miaka michache ijayo.

 “Inabidi sasa tuwe wakali ili isije ikafika wakati tukawa hatuna maji katika nchi yetu”, alitahadharisha Maalim Seif. 

 Amesema katika kudhibiti hali hiyo, serikali itachukua kila aina ya tahadhari kuhakikisha kuwa vianzio vya maji haviendelei kuharibiwa kwa maslahi ya vizazi vijavyo na taifa kwa ujumla.

 Akizungumza katika ziara hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya maji Zanzibar (ZAWA) Dk. Mustafa Ali Garu amesema changamoto kubwa wanayokabiliana nayo kwa sasa ni uvamizi wa ujenzi karibu na vianzio vya maji, hali inayopelekea mfumo wa uzalishaji wa maji kubadilika na kupunguza kwa kiasi kikubwa kiwango cha maji katika chemchem. 

 Kwa upande wake Mhandisi wa Mamlaka hiyo injinia Said Saleh amesema baadhi ya chemchem ndogo ndogo zimeanza kutoweka, na kutaka tahadhari zaidi zichukuliwe katika kudhibiti uvamizi wa vianzio hivyo. 

Amefahamisha kuwa karibu nusu ya kiwango cha maji yamepungua katika kipindi cha miaka kumi iliyopita kutoka katika chemchem za Mtotopepo na Mwanyanya, huku chemchem ya Mtopepo ikiwa na upungufu mkubwa zaidi.Ziara hiyo pia imemshirikisha Waziri wa Ardhi, Makaazi, Maji na Nishati Mhe. Ramadhan Abdallah Shaaban
 
 
Na 
Na Hassan Hamad
Ofisi Ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar

TCRA yawaasa Watanzania kuhamia Digitali

  Naibu Mkurugenzi wa Utangazaji wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCR), Fredrick Ntobi.
Waanzania wametakiwa kujiandaa kuhama katika mfumo wa mabadiliko ya anaelojia kwenda katika mfumo wa digital ambao hadi ifikapo Desemba 31 mwaka huu matangazo ya anaelojia yatazimwa rasmi.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa Naibu Mkurugenzi wa Utangazaji wa  Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA)Bw. Frederick Ntobi amesema kuwa kuanzia Januari 2013 wananchi hawataweza tena kutumia mfumo uliopo wa
sasa wa anaelojia.

Amesema kuwa ili kwenda na utandawazi uliopo hadi ifikapo januari 2013 dunia nzima itakuwa imehama katika mfumo wa kutumia anaelojia katika luninga zao hivyo ni vema wananchi wakaanza kujipanga mapema ili kuhakikisha kuwa kila mtu anafikiwa na huduma hiyo.

Amengeza kusema ku wa ili mfumo huoi ukamilike ni vema jamii ikahakikisha kuwa lazima inakuwa na kifaa kiitwacho kingamuzi ambacho ndicho kinatumika katika kubadilisha mfumo ili kuweza kufanikiwa katika ubadilishaji huo.

Bw Ntobi ametaja faidsa ya kutumia mfumo huo kuwa ni pamoja kuwa na matumizi bora ya masafa ,kupata huduma bora za ziada mfano kulipia bili ya umeme,kutuma pesa pamoja na kupata intenet pindi uwapo kwenye luininga zao.

Pia alitaja faida ingine kuwa ni pamoja na kuongezeka kwa ajira kwa kuwa mfumo utachangia kuongezeka kwa makampuni nmengi ya utangazaji.

MPANGO WA NMB FINANCIAL FITNESS WAENDELEA KATIKA SHULE MBALIMBALI

 Dotto Mbwana, mfanyakazi wa NMB Muhimbili akigawa vijarida vya NMB Financial Fitness kwa wanafunzi wa Shule ya Msingi Muhimbili mpango huo ni kwa ajili ya kuwaandaa wanafuzi kupata uelewa wa masuala ya kibenki mashuleni
Wanafunzi wa Shule ya Msingi Mtibwa wakijisomea kijarida cha NMB Financial Fitness wakati wafanyakazi wa NMB Turiani walipotembelea shule yao
 Wanafunzi wa Shule ya Msingi Muhimbili wakisoma kijarida cha NMB Financial Fitness
 Wanafunzi wa Shule ya Msingi Muhimbili wakisoma kijarida cha NMB Financial Fitness
Meneja wa NMB Muhimbili Janeth Shango akiwasisitizia wanafunzi juu wa kuweka fedha wakiwa na umri mdogo

No comments:

Post a Comment