Wednesday, June 6, 2012

RAIS KIKWETE ACHANGISHA BILIONI 3.2 KATIKA HARAMBEE YA KUCHANGIA MKAPA HIV/AIDS FOUNDATION


ais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akimpongeza Bw. Deo Mwanyika, Makamu wa Rais wa Kampuni ya Barrick Tanzania baada ya kuibuka mchangiaji mkubwa kwa kutoa dola za Kimarekani laki 5 kwa ajili ya kuchangia taasisi ya Mkapa Hiv/Aids Foundation Jumanne Juni 5, 2012 usiku katika hoteli ya Kilimanjaro jijini Dar es salaam. Kushoto ni Rais Mstaafu  wa Awamu ya Pili Alhaj Ali Hassan Mwinyi na kulia ni Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Mzee Benjamin William Mkapa aliyeandaa hafla hiyo iliyoweza kukusanya shilingi bilioni 3.2 na kuvuka malengo ya harambee hiyo kwa asilimia sita
 Rais Jakaya Kikwete, akimkabidhi picha ya kuchora Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya UNDI Consulting Group Limited, Bw Philip Makoka aliyoinunua kwa shilingi milioni 20 wakati wa Harambee ya kuchangia fedha programu ya Mkapa Fellows inayoendeshwa naTaasisi ya Mkapa HIV/AIDS iliyofanyika Dar es Salaam kwenye hoteli ya Kilimanjaro Hyatt  Regency jijini Dar es salaam. Kulia ni mchoraji wa picha hiyo, Bwana Muzu
 Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akisindikizwa  na  Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Alhaj Ali Hassan Mwinyi (kushoto)  na Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Mzee Benjamin William Mkapa baada ya kuwa mgeni rasmi katika harambee ya kuchangia Taasisi ya Mkapa HIV/AIDS foundation na kusaidia  kukusanya shilingi bilioni 3.2 nauvuka malengo ya harambee hiyo kwa asilimia sita.PICHA NA IKULU

MAKAMU WA RAIS DKT BILAL AAGANA NA BALOZI WA CANADA ALIYEMALIZA MUDA WAKE NCHINI

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Balozi wa Canada nchini Tanzania, Mhe. Robert J. Orr, aliyefika Ofisini kwa Makamu Asubuhi ya leo Juni 06, 2012 kwa ajili ya kumuaga rasmi baada ya kumaliza muda wake nchini.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na kumkaribisha Balozi wa Canada nchini Tanzania, Mhe. Robert J. Orr, aliyefika Ofisini kwa Makamu Asubuhi ya leo Juni 06, 2012 kwa ajili ya kumuaga rasmi baada ya kumaliza muda wake nchini.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Balozi wa Canada nchini Tanzania, Mhe. Robert J. Orr, aliyefika Ofisini kwa Makamu Asubuhi ya leo Juni 06, 2012 kwa ajili ya kumuaga rasmi baada ya kumaliza muda wake nchini.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na kumkaribisha Balozi wa Canada nchini Tanzania, Mhe. Robert J. Orr, aliyefika Ofisini kwa Makamu Asubuhi ya leo Juni 06, 2012 kwa ajili ya kumuaga rasmi baada ya kumaliza muda wake nchini. Picha na Muhidin  Sufiani-OMR

ANOTHER DRAW AND TWO MORE LUCKY TANZANIANS WALK AWAY WITH A GENERATOR AND A MOTORBIKE.

Life changing winnings, life changing Experiences, this is all happening with the Under the Crown Campaign.
Today for the sixth week running the lucky draw for the campaign “VUMBUA HAZINA CHINI YA KIZIBO” was held at Serengeti Breweries’ offices in Oyster bay area. 
 
Speaking at the press conference, the Director of marketing, Mr. Ephraim Mafuru said, “We have given away generators, motorbikes and Bajaj’s, we still have more for youTwo weeks ago we gave away a brand new vehicle, Ford Figo and we still have more cars to give away.  We wish to remind all our consumers to participate in this promotion as it is designed with them in mind”.  He also reminded Tanzanians that to participate one must be above the age of 18 years and must be eligible to be part of this exciting promotion that still has about 12 weeks to go.

The Vumbua Hazina Chini ya Kizibo promotional campaign draw is highly supervised and in every draw is done in the highest transparency.  The event every week is graced by the members of the press, the gaming board of Tanzania and other internal and external stakeholders including PUSH mobile who have supplied the mechanics of the game and the reputed PricewaterhouseCoopers who ensures there is no ambiguity at all and that every Tanzanian has a chance to win.

The campaign comprises of prizes worth Tshs 780M in total that include cash prizes of over 380M .    The cash prizes come directly to your phone via Mpesa and other prizes are handed over to the winners at their respective regions at no extra costs including transport etc.
Today the motorbike went to Vicent Lymo 36 Years from  Kibosh  Kilimanjaro region and Deusdedit Njau 22 Years  from  Kiboroloni Moshi  Kilimanjaro region has won a generator.   Serengeti Breweries Limited (SBL) through its high quality premium drinks, Serengeti Premium Lager, Tusker Lager and Pilsner Lager has been running this remarkable campaign that is making huge changes to its customers and  Tanzanians in general.

TAARIFA KUTOKA KWA ZITTO KABWE

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
06.06.2012

YAH: VIPAUMBELE VYA KAMBA YA UPINZANI KWA MWAKA WA FEDHA 2012/2013

Ndg. Waandishi wa Habari

Mwaka 2011/2012 Kambi ya Upinzani Bungeni ilitangaza Vipaumbele vyake katika Bajeti Mbadala ambavyo vilikuwa:

1.    Kupunguza misamaha ya kodi mpaka 1% ya pato la Taifa kutoka 3%

2.    Kupunguza kodi kwenye bidhaa za mafuta ya petrol na dizeli ili kupunguza mfumuko wa bei

3.    Kufuta mfumo wa posho za vikao (Sitting allowances).

4.     Kupeleka sehemu ya tozo ya ujuzi (Skills Development levy-SDL) kwenye bodi ya mikopo ya  elimu ya juu.

Masuala haya pamoja na mengine yalikuwa sehemu ya Bajeti kivuli iliyowasilishwa Bungeni na Kambi ya Upinzani.

Mapendekezo mawili,
(1) Kodi za mafuta ya Petrol na Diseli na
(2) Tozo ya SDL yalikubaliwa na kutekelezwa. Pendekezo la misamaha ya kodi lilikubaliwa  lakini Serikali imeshindwa kulitekeleza na pendekezo la kufutilia mbali posho za vikao halikukubaliwa.

Kambi Rasmi ya Upinzani inataka maelezo ya kina ya kwa nini Serikali imeshindwa kutekeleza ahadi yake iliyoitoa Bungeni kwamba misamaha ya kodi itapungizwa mpaka kufikia 1% ya pato la Taifa. Halikadhalika Kambi ya Upinzani inarejea wito wake wa kufutwa kwa Mfumo wa posho za vikao (sitting allowances).
Serikali imependekeza Bajeti ya Tshs. 15trillioni kutoka Tshs. 13 trillion. Hata hivyo ni dhahiri kwamba Bajeti ya 2011/12 ilikuwa ina changamoto kubwa za utekelezaji. Serikali ieleze itawezaje kutekeleza Bajeti ya 15trillioni?
Katika Bajeti Mbadala ya 2012/2013 Kambi ya Upinzani itajikita katika maeneo yafuatayo na kuishinikiza Serikali kuyatekeleza.

1. Kuendelea kushinikiza kupunguzwa kwa misamaha ya kodi mpaka 1% ya Pato la Taifa. Hivi sasa misamaha ya kodi ni sawa na misaada yote kutoka nchi wahisani, Tshs 1.03 trillioni ni sawa na 3% ya Pato la Taifa.

2. Kuelekeza raslimali fedha kwenye maendeleo vijijini hasa kujenga miundombinu kama barabara za vijijini na umeme vijijini.

3. Kuelekeza fedha za kutosha  kukarabati Reli ya Kati na kufufua njia za Reli za Tanga, Moshi na Arusha.

4. Kuongeza wigo wa kutoza  tozo la ujuzi (Skills Development Levy) ambapo sasa waajiri wote walipe ikiwemo Serikali na mashirika ya umma. Pia kupunguza tozo hili mpaka 4% ambapo 1/3 itaenda VETA na vyuo vya Ufundi na 2/3 itaenda Bodi ya Mikopo ili kukabili changamoto ya mikopo kwa wanafunzi.

5. Kushusha kima cha chini cha kodi ya mapato (PAYE) mpaka 9% ili kuwezesha wananchi wa hali ya chini kubaki na fedha za kutumia na kukuza uchumi.

6. Kuongeza mapato ya ndani na kupunguza mikopo ya kibiashara kwa kuhakikisha mapato ya ndani yanafikia 20% ya pato la taifa, kuongeza nguvu za kisheria na udhibiti ili TRA ikusanye mapato zaidi kwenye kampuni za simu na kwenye shughuli za uchimbaji wa madini, mafuta na gesi.

7. Kutayarisha Taifa kuwa na uchumi wa Gesi.

8. Kupunguza /kufuta kodi kwenye bidhaaa za vyakula kwa muda maalum ili kushusha mfumuko wa bei.

9. Kuweka mfumo mpya wa elimu kwa kushirikisha sekta binafsi katika kutoa elimu kwa ubora zaidi, ikiwemo kuundwa kwa chombo cha Udhibiti wa Elimu(Regulatory authority)

10. Kutoa vipaumbele na unafuu vya kikodi kwa viwanda vya ndani vinavyotumia malighafi za nchni hasa za kilimo na zenye kuongeza ajira kama Korosho,Pamba na Mkonge.

Kambi ya Upinzani itaendelea kufuatilia kwa karibu sana suala la kukua kwa deni la Taifa amabalo limefikia hadi Tshs 22 trillioni na kutaka ukaguzi maalum kuhusu akaunti ya Deni la Taifa.

Kambi ya Upinzani itawekeza kusimamia kwa karibu suala la matumizi yasiyo na tija ya Serikali hasa kwenye  magari na posho mbalimbali na Kwamba  fedha nyingi zitumike kwa miradi  mikubwa ya maendeleo ili kukuza ajira. Halikadhalika namna ya kupta fedha za kutekeleza mpango wa Maendeleo wa Miaka mitano

Asanteni sana!
…………………………….
Zuberi Kabwe Zitto(Mb)
Waziri Kivulu-Fedha na Uchumi.

WAJASILIAMALI 11,WAKABIDHIWA RUZUKU ZA SAFARI WEZESHWA JIJINI MBEYA

  Meya wa Manispaa ya Mbeya, Athanas Kapunga(kulia) akimkabidhi Rose Maluila mashine ya kutengeneza Crips ya kisasa baada ya kufuzu kupata ruzuku za Safari Wezeshwa,makabidhiano hayo yalifanyika Viwanja vya CCM Iloma Mjini Mbeya mwishoni mwa wiki.Katikati ni Meneja wa Bia ya Safari Lager, Oscar Shelukindo
Meya wa Manispaa ya Mbeya, Athanas Kapunga(kulia) akimkabidhi Vumilia Mtweve Viti,Meza,Krti za Bia na Jiko la Kisasa baada ya kufuzu kupata ruzuku za Safari Wezeshwa,makabidhiano hayo yalifanyika Viwanja vya CCM Iloma Mjini Mbeya mwishoni mwa wiki.Katikati ni Meneja wa Bia ya Safari Lager, Oscar Shelukindo
Meya wa Manispaa ya Mbeya, Athanas Kapunga(kulia) akimkabidhi Bahati Mbata Cherehani za kisasa baada ya kufuzu kupata ruzuku za Safari Wezeshwa,makabidhiano hayo yalifanyika Viwanja vya CCM Iloma Mjini Mbeya mwishoni mwa wiki.Katikati ni Meneja wa Bia ya Safari Lager, Oscar Shelukindo
Meya wa Manispaa ya Mbeya, Athanas Kapunga(kulia) akimkabidhi Phares Lyimo Compresor ya kutengenezea Ngoma za kisasa na mashine ya Welding  baada ya kufuzu kupata ruzuku za Safari Wezeshwa,makabidhiano hayo yalifanyika Viwanja vya CCM Iloma Mjini Mbeya mwishoni mwa wiki.Katikati ni Meneja wa Bia ya Safari Lager, Oscar Shelukindo
  Meneja wa Bia ya Safari Lager, Oscar Shelukindo akizungumza na Wajasiliamali,wageni waalikwa na wakazi wa Mbeya wakati wa hafla ya kukabidhi ruzuku kwa wajasiliamali wa Safari Wezeshwa katika Uwanja wa CCM Ilomba Mbeya mwishoni mwa wiki.
  Meya wa Manispaa ya Mbeya, Athanas Kapunga(kulia) akimkabidhi Hellen Mwanguku mashine ya kuwokea mikate baada ya kufuzu kupata ruzuku za Safari Wezeshwa,makabidhiano hayo yalifanyika Viwanja vya CCM Iloma Mjini Mbeya mwishoni mwa wiki.Kushoto ni Meneja wa Bia ya Safari Lager, Oscar Shelukindo.

Rais Dkt.Jakaya Kikwete akutana na viongozi wa Kampuni ya Kilimo ya YARA ikulu jijini Dar es Salaam

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika mazungumzo na viongozi wa kampuni ya kilimo ya YARA  ya nchini Norway inayoshughulika na uzalishaji wa mbolea wakati walipomtembelea ikulu jijini Dar es Salaam leo.Kampuni hiyo ina andaa mipango ya kuzalisha mbolea nchini.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa kampuni ya Kilimo ya YARA ya nchini Norway wakati alipomtembelea ikulu jijini Dar es Salaam leo.(Picha na Freddy Maro- IKULU) )

 Madiwani Wilayani Mbozi Mkoa wa Mbeya wakabidhiwa Piki piki kwa ajili ya utendaji zaidi wa kazi

 Picha ya Pamoja ya Madiwani Muda mchache Baada ya kukabidhiwa Piki piki Hizo
 Mkuu wa wilaya Mbozi akimkabidhi diwani Piki piki
 Hizi ndizo piki piki walizo kabidhiwa Madiwani
 Furaha baada ya kukabidhiwa Piki piki hizo 
Mkuu wa wilaya ya Mbozi wa Tatu kushoto akiongea Kabla ya kukabidhi piki piki 
Picha na Mwandishi wetu aliyepo Mbozi

No comments:

Post a Comment